SABABU ZA AWALI ZA KUKATA RUFAA DHIDI YA UAMUZI WA SPIKA WA TAREHE 9/11/2012 WENYE MWELEKEO WA 'FUNIKA KOMBE'
Na: John Mnyika (Mb)
Baada ya habari kutolewa jana na leo juu ya uamuzi wa Spika kuhusu tuhuma kwamba baadhi wa wabunge na wajumbe wa kamati ya Nishati na Madini walijihusisha na vitendo vya rushwa katika kutekeleza kazi zao za kibunge, nimeulizwa na baadhi ya wanahabari na wananchi kwa simu na kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii sababu za kusimama bungeni tarehe 9 Novemba 2012 mara baada ya Spika kutoa uamuzi huo na kutaka kuomba muongozo.
Nalazimika kutoa ufafanuzi huu nje ya bunge baada ya mkutano wa bunge kuahirishwa bila Spika kunipa fursa ya kusema jambo hili bungeni kwamba nilitaka muongozo wake kwa mujibu wa Kanuni ya 5(1) na 5 (2) kuwa nakusudia kukata rufaa dhidi ya uamuzi wake kutokana na kuwa na maudhui kadhaa yasiyozingatia katiba ya nchi, sheria mbalimbali za nchi, kanuni za kudumu za bunge, maamuzi ya awali ya maspika wa Bunge pamoja na mila na desturi za mabunge mengine yenye utaratibu wa kibunge unaofanana na utaratibu wa bunge letu.
http://wotepamoja.com/archives/10337#.UKIJ5iyx-vk.gmail --
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
0 Comments