Nimekusikiliza ukichangia budget ya mambo ya ndani, mwanzoni nilikuelewa uliposisitiza umuhimu wa viongozi hasa wa kisiasa kutoa matamko yanayo wagawa wananchi hasa kuwagawa kidini,ulichonichanganya ni pale ulipo sema serikali inakosea kuongea na BAKWATA kwani sio chombo kinachokubalika na waislamu wote,inawezekana ni kweli kutokana na utafiti wako lakini pengine unguzitaja taasisi nyingine zilizo omba kuongea na serikali sikakataliwa na ni kwa masuala yapi kwani kama sijakosea nadhani ni serikali hiyohiyo iliyoongea na waislamu ambao sio BAKWATA na kuwapa chuo cha TANESCO kama sija kosea na kuwa chuo cha kiislamu Tanzania.Mimi nadhani ungetoa mfano wa tasisi hizo badala ya kuitaja BAKWATA kutokubalika na kuacha kutaja taasisi nyingine zilizonyimwa haki hiyo ya kuongea na serikali.Vilevile unaposema serikali isijihusishe na masuala ya kidini hukufafanua najua muda wa dakika tano hautoshi lakini nivizuri ukawaeleza watanzania kujihusisha kivipi ili tupate tafsiri sahihi.Mimi binafsi serkali kusaidia taasisi ya kidini kama ya kiislamu kupata eneo la kutoa huduma za kijamii kama elimu(Chuo cha kiislamu ni sahihi) lakini kwa uendeshaji dini pengine inaweza isiwe sahihi.Nahisi badala ya kusaidia kutatua tatizo wewe ndio unamwaga petroli Mh tueleze hata muamsho na vikundi vingine vya kigaidi navyo vipewe nafasi mimi binafsi nadhani sio sahihi,Mwisho tuambie grievancies unazotaka serikali kushughulikia nizipi au ni zile tunazosikia kila siku kwenye mihadhara?
Related Posts
- [wanabidii] Press Releases: Ambassador Sung Kim, Special Representative for North Korea Policy, Travel to Tokyo and Beijing
- [wanabidii] Partisanship and the State of the Union, plus...
- [wanabidii] Africa: Dubai, a key hub for 'Gold' business into the Middle East and Africa
- [wanabidii] What the Mossad (Really) Said, #IAmKnife terror supporters, Bibi to visit D.C. (Obama upset), WhatsApp on the PC, King Tut (broke) - Jan 22, 2015
- [wanabidii] Press Releases: Decker Anstrom To Lead U.S. Delegation to ITU World Radiocommunication Conference
- [wanabidii] Mpango wa BRN Sekta ya Elimu Unamapungufu - HakiElimu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Comments