KIKWETE: CCM KWANZA MTU BAADAE " ....LAZIMA tusome alama za nyakati .Kubwa zaidi tutambue watu wanataka mtu wa aina gani.Au kwa maneno mengine tutambue zaidi wanachukizwa na mtu wa namna gani. Tusipeleke MTU ANAYEAKISI mambo yanayochukiza wanachi...". Nukuu hiyo ni ya Mwenyekiti wa CCM ,Rais Jakaya Kikwete katika hotuba yake ya ufunguzi wa Kikao cha NEC kilichoanza jana Mei 23 na kinatarajia kumalizika leo Mei 24 mwaka 2015. Binafsi mimi katika haya hii isemao ' TUSIPELEKE MTU ANAYEAKISI MAMBO YANAYOCHUKIZA WATU. Nimeielewa kwamba Rais Jakaya Kikwete alikuwa akimaanisha wana CCM wasimteue Kada wake ambaye anaandamwa na tuhuma mbalimbali ambazo zinachukiza watu. Na hakuna ubishi Watanzania hivi sasa wanachukizwa sana na vitendo vya utoaji rushwa na ufisadi, Hadi sasa baadhi watu wanaotajwa tajwa kugombea Urais kupitia CCM wakiwemo madata sita wansoongozwa na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa nwalishatiwa hatiani kwa matendo ya kuvunja Kanuni,kuanza kampeni mapema Februali mwaka 2014 na Mei 22 mwaka huu walimaliza kutumikia kifungo.Hivyo bado wana rekodi ya kifungo kwasababu hukumu ile iliyokuwa ikiwakabili haijawahi kutenguliwa na mamlaka yoyote hivyo hawa wanahesabika ni wafungwa wa CCM waliomaliza kutumikia kifungo. Na miongoni mwa wanaotajwa tajwa kugombea urais kupitia CCM wanaakisi mambo yanayochukiza wananchi. Sasa kwa kwa tafsiri nyepesi ya aya hiyo iliyopo kwenye Hotuba ya Rais Kikwete, ni kwamba Rais Kikwete kwa mamlaka aliyonayayo anawataka wajumbe wa NEC wasimpishe mgombea yoyote wa ngazi ya urais ,udiwani,bunge ambaye anaandwa na tuhuma ,matendo yanayochukiza watu. Kwa nukuu hiyo wale wote wanaotaka kugombea hasa nafasi ya urais ndani ya CCM, muitafakari sana nukuu hiyo na kila mmoja wenu aone 'dongo hilo la Kikwete' linamhusu yeye binafsi kutokana na vitendo anavyovifanya yeye au genge lake? Na kama 'dongo ' hilo linamhusu basi haraka iwezekanavyo aachane na mpango wake wa kugombea urais maana ukimtazama Kikwete wakati akitoa haya hii isemayo ; 'TUSIMPELEKE MTU ANAYEAKISI MAMBO YANAYOCHUKIZA WATU' , alibadilika sura na kuonekana kuwa anachukizwa na hilo, na wale 'Dongo' hilo linalowahusu mjiandae Kisaikolojia maana niwazi hamtasalimika. By Happiness Katabazi Blogg: www.katabazihappy.blospot.com 0716 774494 Mei 24 mwaka 2015. |
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments