[Mabadiliko] Fw: KWAKO KAMANDA MKUU

Friday, July 22, 2022
Nimelikumbuka andiko langu

----- Forwarded Message -----
From: lucas haule <kisacha2003@yahoo.com>
To: Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>; Mabadilikotanzania <mabadilikotanzania@googlegroups.com>
Sent: Tuesday, August 22, 2017 at 09:34:31 AM GMT+3
Subject: KWAKO KAMANDA MKUU

Shikamoo mzee

Wewe ndiye kamanda wa makamanda hapa kwetu kwenye nchi ya urithi.
Mtu mwerevu na shujaa wa mapambano, si mjivuni lakini mweredi. Kwako tunaona tunu ya uafrika na zao bora la nchi takatifu mama Tanzania.

Ni wewe pitio la seminari kule wapikao watu wanyenyekevu, wenye kujua nidhamu, watii na wacha Mungu. Iwe umepata au umeishia niani kabla ya daraja takatifu.

Nina andika waraka huu huku nikijinasibu  kuwa hauta tuma wale vijana watekaji na watesaji kutenda miimo yao.

Nyerere, twamwita Baba wa taifa hili. Alipogombea au kupigania waweza ita kutafuta uhuru wa nchi hii hakuwa na maana ya kuwabagua wahindi, wazungu, waharabu ama watu wengine wasio wa asili ya uweusi.

Wewe si muuaji ( kwa maana kufurahia vifo vya holela) Ni mtoto wa kikurya, mwenye ushujaa wa kweli na si mpiganaji na watu duni, wanyonge, ama wasichana. Hakuna mkurya timamu akafanya upuuzi huu.

Ni wapi mwalimu Nyerere alifikia kuvunja sheria, kanuni, ama katiba kwa kuzuia mtanzania asiende sehemu nyingine ya nchi kushiriki kuijenga nchi?

Somo lipi ukaliunganisha na lipi kule seminari, ulifundishwa, kufanya aliyoyafanya Herode? ( kutaka kuua watoto kwa hofu ya mfalme kunyang'anywa ufalme wake)

Kama kuna kitu kinapandwa, yawezekana hukijui ( moyo wangu waniambia unakijua) Polisi kutumika kama mpinzani wa vyama vingine vya kisiasa na watu wengine wenye mawazo tofauti kuhusu mienendo ya viongozi na uendeshaji nchi. Una/ polisi wanapandikiza UBAGUZI  kwa njia za wazi kabisa.

Nakukumbusha mzunguko wa unyanyasaji - Ukimnyanyasa mtoto leo, kesho mtoto atamnyanyasa mtoto mwingine mnyonge ama wadudu na wanyama walioko nyumbani. ( ukiona mtoto wako anapiga paka, anaua mende bila hofu) akili hata ikiwa ndogo kama yangu jua mtoto amepandikizwiwa ukatili). Muulize Kittila Mkumbo

Kuzuia viongozi wa vyama vingine waisende kushiriki siasa upande mwingine, huu ni ubaguzi mmbaya sana. CCM ambayo kadi zake tunazo mfukoni mwake, haiwezi kupendwa kwa kuzuaia watu/ wananchi wasisikie habari mbadala. Wakitaka hivyo wasikutumie wewe. Linda heshima yako ya leo na hata milele.
Kumbuka; ulizingiziwa tena kwakukosewa heshima mbele ya waziri mkuu kuwa eti, mtu anawasiwasi na wewe unashirikiana na wauza shishi na unga.
Tulipo simama nyuma yako hatukuwa punguani. Ukweli wa wewe tunaujua bila wewe kujiatangaza wala kujipendekeza. Shukrani waziri mkuu alitenda jambo jema. Tunakupenda sana.

Leo polisi Tarime wanamkamata kadada ka watu tena kanaenda kuchangia shule na mabweni. Ni serikali hii haitaki watoto wakike wenye ujauzito au waliojifungua waendelee na shule za serikali. ( unajua vizuri kule mara, mtoto asipoenda shule hata akiwa na miaka kumi na mbili nini kitamkuta akiwa wa kike)
Unataka watoto wa wakurya warudie kuwa wauza ndizi na mabeseni kichwani? Hawa wanaotoa amri hii baada ya miezi kadhaa wataenda makwao nandiyo watakao sema wakurya hawajasoma. Aibu hii itakuwa mikononi kwako.

Nani aliyesema, au maaligani pameandikwa kuwa ccm wanahaki zote kutembea na kufanya lolote katika ardhi ya tanzania, na vyama vingine siyo wa tanzania?

Hivyo vyama vikijinyanyua na kuanzisha mapambano ya kimyakimya, umepanga itakuchukua muda gani kumaliza hilo tatizo?
Unajua ama umejifunza njia mbalimbali za kuondoa uchungu? kama ndiyo unao wataalamu kiasi gani kuondoa uchungu na dhuruma hii inayotokea?
Je, umepanga ukistahafu tukukumbuke kama nani? Yule mpambe wa Idd amini bialamungu au Maliyamumgu wa uganda? Tukukumbe kama Sajenti Samweli do wa Laiberia? Tukukumbuke kama nani, mpenda kutesa wanawake na watoto? mtekaji? mlanyama za watu? mpenda sadaka za dhambi?

Nina amini nawe watambua utu wako, miiko ya kazi yako na tarehe za kustahafu kwako.
Nia yako njema ionyeshe kwa watanzania wote.
Naweza kujifunza kwamba hufurahii hali hii ila unalazimika kwa sababu labda( walioko madarakani ) wanataka hivyo kusudi yakitibuka watangaze hali ya hatari. ( km ni mimi niko tayari kujiuzu kuliko mshahara wa dhambi)

Sina shaka na umahiri wako, hili ni andiko langu mimi nisiye na kitu, mnyonge mwana poli, mtoto wa mpolipoli. Niite haywani jina linitialo nguvu.

Wakatabau chepo la Mwisho. Sifi mara mbili

Share this :

Latest
Previous
Next Post »
0 Comments