huu utenzi!!!!..........................
Uko wapi baba, mwanao mimi nakutafuta/
Ni miaka imepita enzi za baiskeli mpaka sasa kuna Guta/
Njoo upesi baba uwaone wezi wanatupa suluba kimyakimya bila vita/
Ningekutajia majina sema tu moyo unasita.
Wale uliowaacha vijana sasa ni wazee mfano Samweli Sita.
Wale wabunge wako watiifu hawapo tena sasa kuna mafisadi/
Wanataifisha ardhi yako tena hasahasa migodi/
Kisha wanapewa heshma kwa kuchongewa jembe la Gold/
Tuliyemtegemea mtafanana kumbe naye goigoi/
Amekufanana jina tu ila kimatendo bora Toi/
Njoo maramoja baba uturejeshe kwa wakoloni/
Hapa kwenye uhuru tunaish kama motoni/
Sera ya kujuana inawatesa wanazuoni/
Hata waliosoma sana ajira hivi sasa hawazioni/
Yule mwenye kitambi alituletea shule za kata/
Mwenzake amekuja hana jipya ujinga mtupu amepakata/
Heri tumpe faida mchuuzi tuvujishe hli pakacha/
Hawa wapinzani na watawala nao wanafanana kama mapacha/
Bunge lako tukufu sasa wanaimba kwasakwasa/
Wanapeana mipasho waziwazi wanadai hzo ni siasa/
Sheria zimebadilika sasa askari ruksa kufanya mauaji/
Thubutu kuwakemea nawe uende na maji/
Mgambo wa jiji kamgeuza machnga mtaji/
Ushoga na uchangudoa biashara halali katkat ya jiji/
*LEO TUNAMKUMBUKA"
--
Ipyana Lwinga
Email: ipyanalwinga@gmail.com
Mob: +255 757 065577
Skype: ipyana.plwinga
"Mpende Jirani yako kama nafsi yako..."
--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
0 Comments