Dhana ya ukombozi wa mtanzania ilianza tangia wakati wa ukoloni tukiwa bado tunatawaliwa na wazungu. Historia ya ukombozi wa Taifa letu inaanzia nyuma sana, enzi za mababu zetu, akina Mkwawa, Mirambo, Mangi Sina na wengine wengi. Mashujaa hawa walipigania uhuru wa Taifa hili na kuupinga ukoloni na ubeberu, hata kuwa tayari kuifia nchi yao.Mwalimu Nyerere aliendeleza historia ya ukombozi kwa kupinga kwa nguvu zake zote ukoloni na ubeberu mpaka tukafanikiwa kujitawala mwaka 1961. Baada ya uhuru, agenda kubwa ya Taifa ilikuwa ni kujitawala na kujiletea maendeleo yetu.Vijana tunajifunza nini kutoka kwa kizazi cha kina Mkwawa? Walipigana na ukoloni hadi kujitoa maisha yao kwa ajili tu ya Ukombozi; yaani walijitoa sadaka. Halikadhalika, kizazi cha mashujaa wasiotetereka, cha Mwalimu Nyerere, kilipambana kutafuta uhuru wa mtanzania na kufanikiwa kuweka misingi ya ujenzi wa Taifa letu. Hawa mashujaa wote walijitoa sadaka. "They sacrificed their lives for the people of Tanzania".
http://wotepamoja.com/archives/8692#.UHqlcWXLZXg.gmail --
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
0 Comments