[wanabidii] Taarifa ya JWTZ ya kuzindua huduma ya Tiba bure kwa jamii

Friday, August 15, 2014
Jeshi la Ulinzi la Wananchiwa Tanzania (JWTZ), linatarajia kuzindua huduma ya Tiba kwa jamii kuanzia tarehe 15 Agosti 2014 hadi 19 Agosti 2014 kuanzia saa 12:00 asubuhi hadi 12:00 jioni katika viwanja vya Mnazi mmoja. Huduma hizi zinakwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 50 ya JWTZ.

Huduma zitakazotolewa ni pamoja na vipimo vya magonjwa ya Homa ya Ini (Hepatitis B& C), Presha, Kisukari, Huduma za Ushauri nasaha na kupima VVU, Huduma za uchangia damu salama, Macho, Kinywana Koo. Kwa vipimo vya Malaria, matibabu yatatolewa hapo hapo. Huduma zote hizo ni bure.

Nafasi hii itatoa mwanga wakuweza kuona ueledi wa madakitari wetu wazalendo ambao ni matunda yenu.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo anatarajiwa kuwa Waziri wa Afya Dk. Selemani Seif Rashidi. JWTZ linawakaribisha wananchi wote.

Tumelinda, tunalinda, tutalindadaimaTaifaletu Tanzania.


Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203, Dar es Salaam, Tanzania.
KwaMawasiliano zaidi: 0754 - 270136

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Previous
Next Post »
0 Comments