[wanabidii] Katibu Mkuu UVCCM aanza ziara ya siku 14 Kanda ya Ziwa

Friday, December 12, 2014
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Katibu Mkuu wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Ndugu Sixtus Mapunda anategemea kufanya ziara ya siku na nne (14) katika mikoa minne ya Kanda ya Ziwa, ambayo ni Tabora, Shinyanga, Geita na Kagera kuanzia kesho tarehe 12st Dec 2014.

Ziara hii ya kikazi ya Katibu Mkuu inalenga kukagua na kuhimiza ujenzi na uimara wa jumuia ya Vijana katika maeneo husika lakini pia kushiriki kampeni zinazoendelea za uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mnamo tarehe 14th Dec 2014.

Pia, Katibu Mkuu anatarajia kufanya mikutano ya ndani na viongozi wa Jumuiya na Chama, pia kufanya mikutano ya hadhara inayolenga kuingiza wanachama wapya ndani ya jumuiya na chama kwa ujumla.

Kuhimiza wanachama wa chama cha mapinduzi na viongozi kuwaandaa wananchi katika kuipigia kura katiba mpya iliyopendekezwa wakati ukifika.

Ziara hiyo ya Katibu Mkuu inategemea kumalizika tarehe 25th Dec 2014.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments