[wanabidii] APELEKWA HOSPITALI BAADA 'MASHINE' KUSIMAMA KWA SAA 17

Wednesday, October 08, 2014
Mfanyakazi mmoja wa hoteli nchini Uingereza alilazimika kutoa painti mbili za damu (Takriban lita moja) kutoka kwenye uume wake- baada ya kusimama kwa muda wa saa 17 mfululizo.
Madaktari kwanza walijaribu kupunguza kasi ya damu kwa kijana huyo, Jason Garnett, kwa kupiga sindano 24 moja kwa moka kwenye nyeti zake.
Tovuti ya Metro imesema 'mashine' ilisimama kuanzia siku ya Ijumaa asubuhi alipoamka. Kijana huyo, 23, alijaribu kila aina ya njia, ikiwemo kukimbia, na kuoga maji ya baridi sana, kabla ya kupelekwa hospitali na rafiki yake. 
Hospitali iligundua kuwa Garnett alikuwa na maradhi ambayo ni haba kuonekana yajulikanayo kama priapism - ambapo uume husimama bila kukoma. Maradhi hayo hayasababishwi na hamu ya kutaka kufanya mapenzi, lakini iwapo mtu hatopata tiba, inaweza kuharibu uume, imeripoti tovuti ya News.com.au.
Akizungumza na gazeti la The Sun, amesema: "Yaani kuishia hospitali na jambo hili, ni moja ya siku ya aibu zaidi kwangu duniani.
"Kuona wakichoma sindano 'mashine' yangu ilikuwa jambo gumu sana kwangu- kama kutazama filamu ya kutisha. Maumivu yalikuwa asilimia 100." 
Amesema baada ya sakata hilo, nyeti yake ina majeraha 'kibao'.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments