TAARIFA KWA UMMA
TOLEO LA SARAFU YA SHILINGI MIA TANO.
Benki Kuu ya Tanzania ndiyo chombo chenye jukumu la kutoa sarafu
na noti halali (legal tender) zinazotumika nchini. Katika kutekeleza
jukumu hili Benki Kuu hutengeneza noti na sarafu zenye uwiano mzuri
wa thamani (denominations) unaozingatia uwezekano wa zile zenye
thamani kubwa kuweza kugawika katika zile zenye thamani ndogo
ndogo.
Hii hulenga kurahisisha upatikanaji wa chenji na uwezekano wa
wahitaji wa viwango mbalimbali vya bidhaa na huduma kupata
katika mafungu yatakayokidhi mahitaji yao.
Katika kutekeleza jukumu hili, Benki Kuu imetoa toleo jipya la Sarafu
ya Shilingi 500. Hatua hii imezingatia yafuatayo:
* kwamba noti ya shilingi mia tano (500), ndiyo inayotumika
zaidi kwenye manunuzi ya kawaida ya kila siku ya wananchi
wengi kuliko noti nyingine yoyote. Hivyo noti hiyo hupita
kwenye mikono ya watu wengi katika kipindi cha muda mfupi
sana na kuchakaa haraka.
* Noti hizi hukaa katika mzunguko kwa muda mrefu bila
kurejeshwa kwenye mabenki kwa wakati muafaka ili
zibadilishwe zinapokuwa zimefikia ukomo wake.
* Sarafu hukaa kwenye mzunguko kwa miaka mingi zaidi kuliko
noti. Sarafu hii inatambuliwa kwa kuangalia yafuatayo:
* Umbo lake ni la duara lenye michirizi pembezoni, kipenyo
cha milimita 27.5 na uzito wa gramu 9.5
* Ina rangi ya fedha na imetengenezwa kwa madini aina ya
chuma (Steel) na "Nickel"
* Kwa mbele ina sura ya Rais wa Kwanza wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar, Sheikh Abeid Aman Karume na kwa
nyuma ina taswira ya mnyama nyati akiwa mbugani.
* Ina alama maalum ya usalama iitwayo "latent image" iliyopo
upande wa nyuma ambayo ni kivuli kilichojificha. Kivuli hiki
huonesha thamani ya sarafu '500' au neno 'BOT'
inapogeuzwa-geuzwa.
Sarafu hii mpya ya shilingi mia tano (500) inatarajiwa kuingizwa kwenye
mzunguko kuanzia mwezi Oktoba 2014.
Sarafu hii, itakuwa ikitumika sambamba na noti zilizopo sasa za shilingi
mia tano mpaka hapo noti hizo zitakapokwisha katika mzunguko.
Pamoja na taarifa hii; tunawaomba wananchi kuendelea kufuatilia vipindi
mbalimbali vitakavyokuwa vinaeleza jinsi sarafu hii ilivyo na namna ya
kutunza noti na sarafu zetu kwa njia salama.
Ahsanteni Sana.
(source: BOT) 8th september, 2014.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments