Na. Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma.
Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limetoa tamko la kuzuia maandamano ya Chama cha CHADEMA hapo tarehe 18/09/2014 na kuwataka wananchi kuyapuuza.
Akiongea na waandishi wa habari, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishina Msaidizi wa Polisi EMMANUEL G. LUKULA (ACP) alisema kuwa; Kufuatia Viongozi wa CHADEMA kutaka kufanya maandamano kuelekea viwanja vya Ofisi za Bunge Mkoani Dodoma kwa ajili ya kupinga Bunge la Katiba siku ya tarehe 18/09/2014 linaloendelea, kuwa maandamano hayo ni batili na akiwataka wananchi wakazi wa Dodoma kuyapuuza kwa kuwa yanakiuka Sheria iliyoliweka Bunge hilo.
Kamanda LUKULA – ACP alitaja sababu za msingi za kuzuia maandamano hayo kuwa ni:-
Siku ya maandamano ya tarehe 18/09/2014 ni siku ya kazi ikiwa ni pamoja na muda wa maandamano hayo ni masaa ya kazi saa 04:00 asubuhi hadi saa 06:00 mchana yataathili ufanisi wa watu waliopo makazini/maofisini.
Bunge maalumu la Katiba linaloendelea kwa sasa lipo Kisheria na hakuna tamko lolote lililotolewa na Mahakama yoyote kulisitisha, hivyo moja ya kazi ya Jeshi la Polisi ni kulinda Sheria na wale wanaofuata sheria. Hivyo kufanya maandamano yanayopinga Bunge la Katiba ni kukiuka Sheria iliyoliweka Bunge hilo.
Kuna kesi Mahakamani ya kupinga Bunge hilo kuendelea, hadi sasa shauri hilo linaendelea Mahakamani. Hivyo kwa CHADEMA kuandamana ni kuingilia Uhuru wa Mahakama.
Baadhi ya Wilaya barua za kufanya maandamano zimechelewa kufika kwa Wakuu wa Polisi Wilaya kabla ya saa 24 kisheria.
Aidha Kamanda LUKULA – ACP alisisitiza kuwa kwa sababu hizo alitoa wito kwa wananchi wa Dodoma kupuuza maandamano yoyote ya kupinga uwepo wa Bunge la Katiba kwani ni batili. Aidha aliwashauri viongozi wa CHADEMA Mkoa na Wilaya za Dodoma wayasitishe maandamano hayo na wasipo ridhika, wakate rufaa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwa maelekezo zaidi.
-- Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limetoa tamko la kuzuia maandamano ya Chama cha CHADEMA hapo tarehe 18/09/2014 na kuwataka wananchi kuyapuuza.
Akiongea na waandishi wa habari, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishina Msaidizi wa Polisi EMMANUEL G. LUKULA (ACP) alisema kuwa; Kufuatia Viongozi wa CHADEMA kutaka kufanya maandamano kuelekea viwanja vya Ofisi za Bunge Mkoani Dodoma kwa ajili ya kupinga Bunge la Katiba siku ya tarehe 18/09/2014 linaloendelea, kuwa maandamano hayo ni batili na akiwataka wananchi wakazi wa Dodoma kuyapuuza kwa kuwa yanakiuka Sheria iliyoliweka Bunge hilo.
Kamanda LUKULA – ACP alitaja sababu za msingi za kuzuia maandamano hayo kuwa ni:-
Siku ya maandamano ya tarehe 18/09/2014 ni siku ya kazi ikiwa ni pamoja na muda wa maandamano hayo ni masaa ya kazi saa 04:00 asubuhi hadi saa 06:00 mchana yataathili ufanisi wa watu waliopo makazini/maofisini.
Bunge maalumu la Katiba linaloendelea kwa sasa lipo Kisheria na hakuna tamko lolote lililotolewa na Mahakama yoyote kulisitisha, hivyo moja ya kazi ya Jeshi la Polisi ni kulinda Sheria na wale wanaofuata sheria. Hivyo kufanya maandamano yanayopinga Bunge la Katiba ni kukiuka Sheria iliyoliweka Bunge hilo.
Kuna kesi Mahakamani ya kupinga Bunge hilo kuendelea, hadi sasa shauri hilo linaendelea Mahakamani. Hivyo kwa CHADEMA kuandamana ni kuingilia Uhuru wa Mahakama.
Baadhi ya Wilaya barua za kufanya maandamano zimechelewa kufika kwa Wakuu wa Polisi Wilaya kabla ya saa 24 kisheria.
Aidha Kamanda LUKULA – ACP alisisitiza kuwa kwa sababu hizo alitoa wito kwa wananchi wa Dodoma kupuuza maandamano yoyote ya kupinga uwepo wa Bunge la Katiba kwani ni batili. Aidha aliwashauri viongozi wa CHADEMA Mkoa na Wilaya za Dodoma wayasitishe maandamano hayo na wasipo ridhika, wakate rufaa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwa maelekezo zaidi.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments