TAARIFA KWA UMMA
UTAFITI WA MAFUTA NA GESI ASILIA KATIKA MAENEO YA MOROGORO
NA KILIMANJARO
Katika toleo Na. 1734 la gazeti la Jambo Leo la tarehe 10 Juni, 2014 katika
ukurasa wa tatu iliandikwa taarifa iliyokuwa na kichwa cha habari
"Utafiti wa gesi kuinufaisha Morogoro, Kilimanjaro". Taarifa hiyo ilieleza kuwa
wakaazi wa mikoa tajwa watanufaika na ugunduzi wa mafuta na gesi uliofanywa
na Kampuni ya Swala katika maeneo hayo.
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linapenda kuwafahamisha
wananchi kuwa taarifa ya kwamba Kampuni ya Swala imegundua gesi na mafuta
katika maeneo ya Morogoro na Kilimanjaro sio sahihi. Ugunduzi wa mafuta
hufanyika tu baada ya kuchimba kisima cha utafiti na hatimaye mafuta au gesi
iweze kutoka yenyewe kutoka ardhini. Hatua ya kuchimba kisima cha utafutaji
hutokana na tafiti mbali mbali za awali za mitetemo ya ardhi na kubaini kama
maeneo hayo yana uwezekano wa kuwa na mafuta au gesi ama la. Hata kama
eneo linaonesha dalili nzuri za awali ni lazima sehemu hiyo ichimbwe na matokeo
yake ni kuwa na ugunduzi au la. Vilevile ugunduzi huo lazima uonyeshe kutoa
kiasi cha rasilimali ambacho kinaweza kuzalishwa kibiashara (economically
viable).
Kazi zilizofanyika mpaka sasa na Kampuni ya Swala katika maeneo ya Morogoro
– Kilosa na Pangani - Kilimanjaro ni utafiti wa awali wa kukusanya takwimu za
mitetemo na kubaini kama maeneo hayo yana kina (thickness) cha kutosha cha
miamba tabaka ambayo utafiti wa mafuta na gesi unaweza kufanyika. Hivyo
utafiti wa kina unaendelea ili kubaini kama kuna miamba mashapo (prospects) ya
kutosha kwa ajili ya kuchimba kisima cha utafiti. Uchimbaji wa kisima hicho
unaweza kutoa mafuta au/na gesi au maji matupu. Hatua ya uchimbaji visima
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments