[wanabidii] Taarifa ya kusitishwa mkutano wa hadhara Zanzibar

Friday, April 18, 2014
YAH: TAARIFA YA KUSITISHWA MKUTANO WA HADHARA

Naomba urejee barua yangu Kumbu. Nam. W/MGH/SO/7/2/A/4 ya tarehe 17 Aprili, 2014 inahusika.

Ninakujulisha rasmi kuwa mkutano huo uliokuwa ufanyika kesho tarehe 19 Aprili, 2014 hapo Viwanja ya Demokrasia Kibanda Maiti umesitishwa kwa sababu za 
KIUSALAMA WA NCHI.

Kwa barua hii unatakiwa kuwajulisha Wanachama na wapenzi wote wa Chama kuwa watulivu kwa muda huu, hadi hapo hali itakapo ruhusu kufanyika tena kwa Mkutano huo.

Tafadhali nawasilisha.

RAMADHANI S. NGAMIA - SSP
MKUU WA POLISI,
WILAYA YA MAGHARIBI UNGUJA.


------------ Mwisho wa kunukuu taarifa ya sitisho hilo. ------------


Katika taarifa ya habari iliyosomwa saa 2 usiku wa leo kupitia TBC, imeelezwa kuwa Jeshi la Polisi Zanzibar limesitisha mikutano yote ya hadhara ya vyama vya siasa visiwani humo.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame, wakati alipokutana na viongozi waandamizi wa vyama vya CCM na CUF katika makao makuu ya Jeshi la Polisi, Ziwani, Zanzibar.

Kabla ya kutolewa tamko hilo CUF ilipanga kufanya mkutano kama ilivyoelezwa hapo juu, wakati UV-CCM ilipanga kufanya mkutano wa hadhara keshokutwa, Jumapili katika eneo la Mabata.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments