[wanabidii] kuhusu hafla ya kumuaga Mstaafu IGP Mwema

Thursday, February 13, 2014
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Jeshi la Polisi nchini, linapenda kuufahamisha umma kuwa, mnamo tarehe 15/02/2014 siku ya Jumamosi katika viwanja vya Polisi Barracks, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam, kutakuwa na hafla ya kumuaga IGP Mstaafu Said Alli Mwema kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana.

Katika hafla hiyo, kutakuwa na mambo mbalimbali yaliyoandaliwa ikiwemo gwaride maalum la 
heshima.
Ikumbukwe kuwa, katika kipidi chake cha uongozi wa Jeshi la Polisi, IGP Mstaafu Said Alli Mwema alishirikiana vyema na wananchi wa kada zote wakiwemo wadau mbalimbali wa amani, hususani katika dhana ya Ulinzi shirikishi na Polisi Jamii. Jeshi la Polisi nchini kwa kulitambua hilo, linatumia fursa hiyo kuwakaribisha wananchi wote kuhudhulia hafla hiyo.

Aidha, IGP Mstaafu Said Alli Mwema katika uongozi wake alianzisha na kusimamia mifumo mbalimbali ya kuzuia na kukabiliana na uhalifu hapa nchini ikiwemo maboresho ndani ya Jeshi la Polisi, ili kuhakikisha Jeshi linafanya kazi kwa weledi, usasa na ushirikiano na wananchi.

Imetolewa na:

Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

Share this :

Related Posts

0 Comments