Mnaojua 'umri wa mtu kwa kumwangalia sura. Naomba mtujuze.
------
Klabu ya Lazio imesisitiza kuwa mmoja ya wachezaji wao-Joseph Minala wa Cameroon ana umri wa miaka kumi na saba kama alivyosema baada ya ripoti kusambazwa kuwa ana miaka arobaini na moja.
Klabu hiyo imesema kuwa cheti cha kuzaliwa cha mchezaji huyo kilikuwa halali.
Minala, ambaye ameshiriki katika mashindano ya vijana chipukizi katika klabu hiyo, pia alitoa taarifa akikana madai kuwa aliliambia mtandao moja wa Kiafrika kuwa alikuwa amedanganya umri wake.
Sakata hiyo sasa huenda ikahujumu mchezo wa Minala ambao katika miezi ya hivi karibuni imekuwa ikiimarika na huenda akakosa fursa ya kujiunga na vilabu vingine endapo mzozo huo utaendelea.
Shirikisho la mchezo wa soka nchini Italia, halijasema lolote kuhusu suala hilo sawai na shirikisho la mchezo wa soka nchini Cameroon.
Katika miaka ya hivi karibuni wachezaji wengi wa Kiafrika wameshutumiwa kwa kudanganya umri wao ili kushiriki ligi ya vijana chipukizi ili kuimarisha nafasi yao ya kujiunga na vilabu vya ulaya.
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la 'Mabadiliko'.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com
MUHIMU KWA WANACHAMA WOTE: Jukwaa hili litafungwa hivi karibuni hivyo hii ni taarifa ya Mwisho kwako kuhakikisha unajisajili www.mabadiliko.com
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mabadiliko Forum" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
To post to this group, send email to mabadilikotanzania@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 Comments