JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA OFISI YA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA: TAARIFA YA AJALI YA MOTO KATIKA OFISI ZA CHADEMA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA OFISI YA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA: TAARIFA YA AJALI YA MOTO KATIKA OFISI ZA CHADEMA
Ndugu wanahabari, mnamo tarehe 03/12/2013 muda wa saa 5:00 asubuhi, polisi mkoani hapa tulipokea taarifa juu ya kuchomwa moto kwa jengo ambalo lina ofisi za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) zilizopo mtaa wa Ngarenaro, Halmashauri ya jiji la Arusha.
Mara baada ya taarifa hiyo askari walikwenda katika eneo la tukio na kukuta moto umezimika. Jengo hilo ambalo lina uzio mrefu wa matofali na geti moja la mbele lina ofisi tatu za chama hicho ambazo ni ofisi za wilaya, mkoa na Kanda ya Kaskazini ambazo zinatumia bafu na choo kimoja.
Aidha uchunguzi uliofanywa na polisi kwa kushirikiana na idara ya zimamoto imegundua mambo yafuatayo:-
Kufuatia tukio hilo jeshi la polisi bado linaendelea kuwahoji mlinzi wa ofisi hizo Kitumbwizi s/o Bahati pamoja na Katibu muhtasi Jenifer d/o Mwasha, huku upelelezi zaidi juu ya tukio hilo ukiendelea.
Asanteni kwa kunisikiliza.
IMETOLEWA NA KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA,
KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI (ACP) JAPHET LUSINGU
TAREHE 04/12/2013.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 Comments