[wanabidii] Marehemu Mzee Karume ana haki ya kuitwa BABA wa TAIFA la Tanzania – Mansoor Yussuf Himid - Mwanzo

Thursday, November 15, 2012
Na Mansour Yussuf Himid


Leo nami nimeamua kutoa mawazo yangu kupitia kwenye ukumbi huu. Kwa wale wasionifahamu mimi ni Mansoor Yussuf Himid nimezaliwa Novemba 3, 1967, kisiwani Unguja. Ni Mzanzibari kwa mama na baba. Kama walivyo Wazanzibari wengine, wazee wangu pia wana asili ya pande mbili – Bara na Arabuni. Baba yangu mzazi ana asili ya Bara ambapo upande wa baba yake ni Mnyasa na upande wa mama yake ni Mmanyema. Na mama yangu ana asili ya Arabuni (Oman), lakini ni mseto wa aina yake maana ana damu ya Kimanyema, Kisomali, na Kingazija. Hali hii si ya ajabu kwa Wazanzibari, bali ni kawaida tu na ndio hali inayotutambulisha Wazanzibari.


Mimi ni Mtanzania kama walivyo wazee na ndugu zangu na wanangu na mke wangu Asha Abeid Amani Karume, kama unajiuliza Karume yupi ni huyo huyo unayemfikiria wewe ni Marehemu Abeid Amani Karume, Baba wa Taifa la Zanzibar , mungu amlaze pema peponi na amsamehe kwa mapungufu yake na amjaalie aendelea kutajwa kwa kheri na wema kama anavyo tajwa sasa.


Marehemu mzee Karume ana haki ya kuitwa Baba wa Taifa la Tanzania pia na wala mshishangae kwani Marekani Taifa la kupigiwa mfano kwa historia na misingi yake imara ya haki za binadamu,demokrasia na utawala bora , wana baba wa Taifa (Founding fathers) zaidi ya mmoja.


Kwa wengine nikiwemo mie kutothaminiwa kwa marehemu Bwana Abeid Amani Karume kwa kuitwa muasisi tu tena wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wala sio Nchi au Taifa la Zanzibar au Tanzania ni kutothamini mchango wake katika kuasisi Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani bila ya Zanzibar hakuna Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ni sehemu ya kero za Muungano wetu.


Tuelewe kuwa kwa kumthamini marehemu Sheikh Abeid Amani Karume, hatuondoshi nafasi ya Marehemu Mwalimu Julius kambarage Nyerere hata kidogo,nafasi ya Mwalimu ni kubwa mno (iconic) kwa wengine iliotukuka (saintly) sio tu kwa Tanzania na Afrika bali mwenyezi mungu amemjaalia Mwalimu kuthaminiwa na kupendwa na mataifa duniani kote,mpaka hii leo miaka kadha baada kufariki kwake, sababu za kupendwa kwa Mwalimu akiwa miongoni mwa viongozi wachache duniani wenye hadhi kama yake ni nyingi kwa leo si dhamira yangu kueleza wasifu wa Marehemu Mwalimu Nyerere.

http://wotepamoja.com/archives/10478#.UKUq0k5ySPc.gmail

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

Share this :

Related Posts

0 Comments