[wanabidii] This must be good news for our Bwana Mobhare Matinyi!!!

Wednesday, October 03, 2012
Hi All,
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi Balozi Seif Ali Iddi, amesema serikali ya Zanzibar imeshajitosheleza katika mfumo 
wa serikali yake na haina haja ya kuwa na serikali ya Mkataba kwani kufanya hivyo ni sawa na kutaka kuvunjika kwa Muungano wa Tanzania.
Balozi Seif, alisema muundo wa serikali ya Zanzibar tayari umetoa fursa ya kuwa na vyombo muhimu vya juu ambavyo vimeweza kuunda serikali 
na hakuna haja ya kutaka kuwapo kwa serikali ya Mkataba ambayo ni sawa na kuuvunja Muungano. Akifafanua kauli hiyo Balozi Seif alisema mfumo 
wa serikali ya Zanzibar ndani ya Katiba umeruhusu kuwa na Katiba yake, Baraza la Wawakilishi, Muhuri, Bendera, Mawaziri, Wawakilishi na Wabunge 
jambo ambalo tayari mfumo huo umejitosheleza.




Share this :

Related Posts

0 Comments