[Mabadiliko] " Ewe Majaliwa Mwema, Hakikisha Unawatokomeza Panya Hao Wa Bandarini.."

Saturday, December 05, 2015


Ndugu yangu Majaliwa Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Vinaonekana, vita unavyopigana kuwakomboa wanyonge walio wengi wa nchi hii.
Kazi unayoifanya hadi sasa inadhihirisha Rais wa Jamhuri, John Magufuli, hakukosea katika kulichagua ' tingatinga' la ukweli la kumsaidia kwenye kazi yake ya Urais.

Hapo bandarini yaonekana kuna mashimo mengi ya panya wanaotafuna mapato ya nchi. Na wengine ni mapanya buku mithili ya ukubwa wa sungura. Eti wanasema ' Bandari Kavu'. Kumbe, zimejaa mashimo ya panya. Iko wapi NASACO ya Watanzania? Miaka 54 ya Uhuru kwanini tushindwe kuendesha wenyewe bandari ya majini na nchi kavu badala ya kuwaachia panya wafanye kazi hiyo?

Ewe Majaliwa Mwema, vita ya panya wa bandarini kamwe isiwe na matokeo ya kutoka sare. Pambana na panya wezi na wenye kuficha mali zilizoibiwa na panya wezi wenzao.

Na ukitoka hapo bandarini na ushindi wa jumla, basi, utasonga mbele ukiwa na nguvu nyingi zaidi, na umma ulio nyuma yako, katika kumsaidia Rais wa Jamhuri kwenye vita ya pili ya ukombozi wa kiuchumi kwa nchi yetu tuliyozaliwa na tunayoipenda.

Wajumbe mnakaribishwa kuchangia...

Good morning.

Maggid,

Iringa.

--
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la 'Mabadiliko'.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com
 
 
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mabadiliko Forum" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
To post to this group, send email to mabadilikotanzania@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania.
To view this discussion on the web visit https://groups.google.com/d/msgid/mabadilikotanzania/CAMD-ye5O33NchCEPn_s5E2JXdXw5iTpUU3YocMvBzFYmFCBNng%40mail.gmail.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments