NA SAMWEL SASALI
Kwa mfano umenasa meseji kwenye simu ya mumeo akiwekeana ahadi na mwizi wako kwamba wakutane gesti fulani wakaibanjue amri ya sita. Bila mumeo kujua wewe ukaandaa majeshi yako na siku ya tukio, mumeo akiwa na mwizi wako gesti, wakiwa hawajui hili wala lile, mnawafumania, picha za ushahidi zinapigwa, mashahidi wanaona na mtaa mzima unajua.
Au umegundua kuwa mkeo anatoka na jamaa wa mtaa wa pili wewe ukiwa umesafiri. Unaamua kumdanganya mwenzi wako kwamba unasafiri na kuacha wapelelezi wa siri wafuatilie nyendo za mkeo.
Unapoondoka tu, anawasiliana na mchepuko wake, wanapanga kukutana na kwa kuwa kuna wapelelezi umewaacha, wanakutonya kila kitu na hatimaye mnafanikiwa kuwanasa wakiwa eneo la tukio.
ULIJIANDAA KIHISIA KABLA YA KUFUMANIA?
Bila shaka umeanza kupata picha ninachotaka kukizungumzia hapa. Je, katika mifano ya hapo juu ya mafumanizi ya kupangwa, wakati unaandaa mipango ya kumfumania mwenzi wako, kichwani mwako ulikuwa unawaza nini? Ulikuwa umeshajiandaa kihisia?
Ulikuwa unataka ukimfumania umpe au udai talaka na huo ndiyo mwisho wa uhusiano wenu au ulikuwa unataka kuhakikisha kama ni kweli? Ulikuwa unataka kumkomoa mwenzi wako au mwizi wako kisha maisha yaendelee kama kawaida?
Ni ukweli ulio wazi kwamba hakuna kitu kinachoumiza moyo kama pale unapogundua kuwa mwenzi wako ana uhusiano na mtu mwingine. Hata kama unahisi tu, moyo huwa unaumia sana.
Yote tisa, kumi hakuna kitendo kinachoumiza au kinachoweza kukufanya ukaathirika mno kisaikolojia maisha yako yote kama kumfuma laivu mwenzi wako akiwa kitandani na mtu mwingine. Awe na nguo au asiwe na nguo, kitendo cha kuwafuma wakiwa wawili tu chumbani, kinaweza kukufanya ukatamani ardhi ipasuke na kukumeza.
Hakuna lugha nyepesi inayoweza kutosha kuelezea maumivu yake, wale waliowahi kuwafumania wenzi wao watakuwa wananielewa vizuri zaidi. Ninachotaka tujadiliane na wewe msomaji wangu ni hiki:
Je, kuna umuhimu wa kumuandalia fumanizi mwenzi wako wakati bado unampenda na unataka muendelee kuishi pamoja, kulea watoto na kutimiza ndoto zenu? Naomba uwe huru kutoa mawazo yako kwa namba za hapo juu halafu wiki ijayo tutaendelea kuangalia mawazo ya kila mmoja na mwisho kufikia hitimisho.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments