[Mabadiliko] ICC yatupilia mbali kesi ya Kenyatta

Friday, December 05, 2014
Mahakama ya kimataifa ya ICC imetupilia mbali kesi ya jinai inayomkabili Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Mwendesha mkuu wa mashitaka Fatou Bensouda ameondoa kesi dhidi ya Kenyatta ambaye alidaiwa kutenda uhalifu dhidi ya binadamu wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007/2008.
Mahakama ilikuwa imempa Bensouda wiki moja kuamua ikiwa ataendelea na kesi dhidi ya Kenyatta au la inagwa alisema muda huo haukutosha kwake yeye kuandaa ushahidi zaidi dhidi ya Kenyatta.
Kenyatta alishtakiwa kama mshukiwa mkuu wa ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007/2008 akituhimiwa pamoja na William Ruto ambaye ni naibu Rais kwa kutenda uhalifu dhidi ya binadamu.
Zaidi ya watu elfu moja waliuawa wakati wa ghasia hizo. Uhuru alikuwa mtu maarufu zaidi kufikishwa mahakamani na pia mshukiwa mkuu kwani alifikishw amahakamani akiwa Rais aliye mamlakani.
Hili ni pigo kubwa kwa upande wa mashitaka, wengi wlaioana keshi dhidi ya Kenyatta kama mtihani mkubwa katika historia ya mahakama hio.
Upande wa mashitaka ulitaka mahakama kuupatia muda zaidi ili upate ushahidi zaidi,dhidi ya Kenyatta kama vile taarifa za akaunti yake ya benki.
Upande wa utetezi uliteta kuwa ikiwa hakuna ushahidi wa kutosha kesi hio inapaswa kutupiliwa mbali.

--

*Lukelo Felix Mkami Mwipopo
(Computer Programmer/Facilitator)
Mob: +255 655 227507,+255 758717356
Skype: lukelo.mkami


--
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la 'Mabadiliko'.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com
 
 
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mabadiliko Forum" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
To post to this group, send email to mabadilikotanzania@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania.
To view this discussion on the web visit https://groups.google.com/d/msgid/mabadilikotanzania/CAErTtmUqY_wdp7OyJFQpmp_rjST0uQOZXzsj-2sL0KRx3w9ryg%40mail.gmail.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments