[Mabadiliko] Ahadi za JK 2010 - 2015 - Tufanye Tathmini Ndogo

Saturday, July 12, 2014
Ni Takribani mwaka mmoja tu sasa umebaki ili kutimia ile miaka mitano ya utawala wa JK. Na nilipojaribu kuingia kwenye kumbu kumbu zangu, nikaamua kuibuka na vitu vilivyowafanya watanzania wakaamua kumchagua JK kuongoza tena. TUjadili, ni ahadi ipi kati za hizi imetimia, na kwa ubora gani? Maana kutimia tu si hoja, hoja ni ufanisi, na ubora wake kwa waahidiwa!

AHADI - ALIITOA AKIWA WAPI...

1.      Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa - Nzega, Tabora

2.      Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda - Tanga mjini

3.      Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria - Igunga

4.      Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU) - Shinyanga

5.      Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini - Dodoma

6.      Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono - Dodoma mjini

7.      Kuwapatia trekta wakulima - Kata ya Mrijo, Dodoma

8.      Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi - Kagera

9.      Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi - Kagera

10.  Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba - Bukoba Mjini

11.  Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini

12.  Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda - Kagera

13.  Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme - Kagera

14.  Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu - Kagera

15.  Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino - Mbeya

16.  Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba - Kagera

17.  Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali

18.  Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika - Mwanza

19.  Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu - Mwanza

20.  Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani - Geita

21.  Kulinda muungano kwa nguvu zote - Pemba

22.  Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa - Morogoro

23.  Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa - Mbeya mjini

24.  Kujenga bandari Kasanga – Rukwa

25.  Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea

26.  Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira - Mbeya

27.  Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama - Tanga

28.  Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini - Iringa

29.  Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani – Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi - Dar es salaam - Same mkoani Kilimanjaro

30.  Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same - Same Mjini

31.  Kuboresha barabara za Igunga - Tabora

32.  Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu - Kisesa Magu

33.  Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya - Mbeya Mjini

34.  Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) - Hydom Manyara

35.  Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa - Musoma

36.  Kulinda haki za walemavu - Makete

37.  Kujenga baabara ya Njombe - Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109 - Iringa mjini

38.  Kujenga barabara Musoma – Mto wa Mbu Arusha - Arusha

39.  Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini

40.  Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma – Kaliua,Tabora

41.  Kukarabati barabara ya Arusha Moshi - Arusha Mjini

42.  Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa, mpaka Singida - Dodoma

43.  Kuwafidia wanakijiji ng’ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009 - Longido

44.  Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria - Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga

45.  Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha – Arusha mjini

46.  Kukopesha wavuvi zana za kilimo - Busekera, Wilaya ya Musoma

47.  Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido - Longido

48.  Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro

49.  Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri - Mbulu mkoani Manyara

50.  Kusambaza maji nchi nzima - Babati vijijini

51.  Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015 - Babati vijijini

52.  Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha - Iringa

53.  Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika - Iringa

54.  Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania - Iringa

55.  Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi -Ifunda

56.  Kutokomeza malaria 2015 - Bunda, mkoa wa Mara

57.  Kuwapa wanawake nafasi zaidi - Kilolo, Iringa

58.  Ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii - Kibandamaiti Mjini Zanzibar

59.  Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa - Kibandamaiti mjini Zanzibar

60.  Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada - Kibandamaiti

61.  Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay - Ruvuma

62.  Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 - Mbambabay Ruvuma

63.  kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) – Ruvuma

64.  Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania – Ruvuma

65.  Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam

66.  Mtwara kuwa mji wa Viwanda – Mtwara

67.  Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu - Kibaha

68.  Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa - Kibaha

69.  Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda - Kibaha

--
Ipyana Lwinga
Email:    ipyanalwinga@gmail.com

"Mpende Jirani yako kama nafsi yako..."

--
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la ‘Mabadiliko’.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com
 
 
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mabadiliko Forum" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
To post to this group, send email to mabadilikotanzania@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania.
To view this discussion on the web visit https://groups.google.com/d/msgid/mabadilikotanzania/CAPd8eK9y826OmfvLPUUQcXFxSx%2BsRkdDDQFy1S9Wh_e%2BWBq73Q%40mail.gmail.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments