Na Frank Mvungi- Maelezo
KITUO cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimefanikiwa kusajili miradi 9,442 tangu kuanzishwa kwake hadi 2013.
Hayo yamesemwa na Meneja Uhusiano wa TIC, Pendo Gondwe wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
Gondwe alisema kuwa Watanzania wamekuwa na muamko katika uwekezaji ambapo katika miradi yote miradi ya Watanzania ni asilimia 52 na 25 ni miradi inayomilikiwa kwa ubia kati ya wageni na watanzania.
Aliongeza kuwa asilimia 23 ni miradi iliyowekezwa na wageni kutoka mataifa mbalimbali ambapo alisema miradi ambayo inaongoza kwa uwekezaji ni Kilimo, Maliasili, Miundombinu, Nishati, viwanda na biashara, Usafirishaji, Elimu, Afya, Miundo mbinu na madini.
Alisema TIC inawahamasisha Watanzania kujitokeza kuwekeza katika miradi mbalimbali ili kusaidia katika kukuza uchumi wa Taifa.
Gondwe alisema TIC imekuwa na utaratibu wa kuhamasisha wananchi kushiriki katika uwekezaji katika sekta nmbalimbali ambapo kituo hicho kimekuwa kikitumia mikutano na makongamano kuhamasisha wananchi kusajili miradi yao.
Kituo cha uwekezaji kinatoa huduma mbalimbali kwa ajili ya wawekezaji wa ndani kupitia dirisha moja yaani ONE STOP CENTRE ikiwemo kuandikisha kampuni, kujisajili na VAT, TIN, na leseni mbalimbali.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments