[wanabidii] JK AISHTUA KAMBI YA LOWASSA,NI MTAFUTAANO SASA

Saturday, February 08, 2014
Kikwete aishtua Kambi ya Lowassa
Na Njenga wa njenga

KAULI ya rais Kikwete aliyoitoa kwenye mkutano wa baraza la vyama vya siasa lililokutana juzi kujadili maadandilizi ya bunge la katiba,kwamba watu wasiishie kubishana kwamba ni serikali tatu au mbili badala yake watazame na sifa zamgombea  imeishtua kabi ya Lowassa.

Kikwete alionenkana kuwashangaa wale wanaishia kubishana kwamba katiba mpya itambue serikali mbili  au tatu badala ya kutazama masuala ya msingi ambayo yatakuja kuleta shida wakati wa utekelezaji wake.

"suala hapa siyo kubishana kwamba ni serikali tatu au mbili …yapo mambo mengi ya msingo ambayo kama msipoyaangalia yatakuja kuleta shida wakati wakuitekeleza katiba hiyo……………..kwa mfano rasmi inasema muda wa kugombea ubunge ni vipindi vitatu na mgombea urais sharti awe na sifa ya kugombea ubunge kwanza  hivyo unaweza kukuta umewekeza kwenye urais ikifika kipindi unakwenda kuchukua fomu ya urais unaambiwa kuwa huna sifa unaanza kuilaumu  katiba mpya……
……..  
Hiyo ndio kauli inayotafsiriwa sawa   na kurusha jiwer kwenye kichanga cha suala  ambapo  kila suala hutoka kwa kasi kwani ilionekana kumlenga Sahawia Lowassa   ambaye kwa mjibu wa Rasimu  ya katiba mpya kama itapita ilivyo hatakuwa  na sifa ya kugombea urais kwasababu hatakuwa na sifa yakugombea   ubunge  baada ya kuvuka  vipindi vitatu  ya kugombea ubunge.

Hiyo ndio kauli ambayo imeawaamsha wafuasi wakeambao ni wajumbe wabunge la  katiba  kuapa kuipigania hadi ibadilishwe…   

Share this :

Previous
Next Post »
0 Comments