[wanabidii] Taarifa ya Mkurugenzi wa VODACOM kuhusu kukosekana kwa huduma ya M-Pesa 21.09.2013

Monday, September 23, 2013
Tunapenda kuwaomba radhi wapendwa wateja wetu, washirika wetu na benki zote pamoja na wananchi wote kwa ujumla kwa kutoweza kutumia huduma yetu ya M-pesa kutokana na kazi ya kuboreshwa  kwa mtandao wa huduma ya M-Pesa. Kazi hiyo ilipangwa kufanyika  kuanzia saa 6 usiku na kumalizika saa kumi alfajiri siku ya  tarehe 21 Septemba, 2013.
 
Kazi ya uboreshaji wa mtandao huo ilikwenda vizuri, lakini mabadiliko hayo yalipelekea kutokea kwa matatizo kadhaa ya
kiufundi ambayo yalidumu kwa muda wa saa 8, hali  ambayo iliyotulazimu kusitisha baadhi ya huduma za mtandao wa M-Pesa.
 
Mafundi wetu walifanya kazi kwa bidii na umakini mkubwa na hatimaye waliweza kutambua na kutatua chanzo cha  matatizo hayo yaliyosababisha kusimama kwa baadhi ya huduma za M-Pesa nchini. Mtandao wa huduma za M-Pesa ulioboreshwa ulitengemaaa na kurudi katika hali yake ya kawaida siku hiyo hiyo saa 11:30 jioni.
 
Kwa mara nyingine tena ninaomba niwatake radhi wateja wetu na washirika wetu wote pamoja na jamii kwa ujumla kwa usumbufu walioupata kutokana na kutopatikana kwa  huduma za M-Pesa nchini.  Aidha,  ninawashukuru nyote kwa uaminifu wenu wa kuendelea kuziamini na  kuzitumia huduma za M-Pesa kukidhi mahitaji yenu ya  kila siku.
 
Rene Meza
Mkurugenzi Mtendaji
Vodacom Tanzania Limited


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

Share this :

Related Posts

0 Comments