[wanabidii] Shukrani kwa wote !

Monday, September 16, 2013
Ndugu, Jamaa na Marafiki !

Nachukua nafasi hii kuwashukuru wote kwa jinsi mlivyoshirikiana nasi kwa hali na mali katika sherehe ya mwisho duniani ya baba yetu mpendwa Wakili Israel Magesa (RIP).

Kama familia hatuwezi kutaja majina ya watu na taasisi moja moja ila tunatoa shukrani za dhati kwa wote na kwa ujumla tunaomba mzipokee.

Marehemu alikuwa ni mtu aliyethamini watu wote na kuwasaidia zaidi wale wasio na uwezo, alithamini sana elimu na aliamini kupitia elimu basi tutaweza kuendeleza nchi yetu kwa kasi kubwa zaidi. Alikuwa ni mchapa kazi, mwenye uzalendo wa hali ya juu kwa Taifa lake na siku zote alikuwa akijali maslahi ya wengi na hakuchoka kufanya kazi kwa bidii na maarifa yake yote, licha ya umri aliokuwa nao na hata siku anafariki ghafla alikuwa anaenda kazini kufanya kazi.

Hivyo basi tunaomba tuendeleze mazuri yote aliyaanzisha au aliyokuwa akiyafanya kwa faida ya jamii yetu na Taifa letu kwa ujumla.

Kila mmoja atimize wajibu wake kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa na kwa pamoja tunaweza kujenga Tanzania bora zaidi ya tuliyoikuta.

Mungu awabariki wote na sasa tuendelee na ujenzi wa Taifa, tudumishe umoja, mshikamano na amani kwa Taifa letu.

Mungu ibariki Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Phares Magesa,
Kny: familia ya Marehemu I.H.M.Magesa,
----------------------------------------------------------



Sent from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel Tanzania.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

Share this :

Related Posts

0 Comments