[wanabidii] Takwimu za Serikali za mahabusu, wahukumiwa wa kesi za dawa za kulevya

Tuesday, August 20, 2013
Imeandikwa na Eleuteri Mangi — Serikali  imeanzisha mkakati  wa  kutokomeza wimbi la tatizo la dawa za kulevya nchini kwa kudhibiti viwanja vya ndege na  sehemu mbalimbali za mipakani  zinazotuhumiwa kupitisha dawa za kulevya. 

Hayo yamesemwa na Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Assah Mwambene leo jijini Dar es salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara hiyo: "Kwa yeyote aliyekuwa anafikiria kufanya biashara ya dawa za kulevya ajue muda wake umekwisha" alisema Mwambene. 

Mwambene alisema kuwa tatizo hili litakuwa historia  kwani ulinzi umeimarishwa, hivyo ametoa rai kwa
mtu yeyote mwenye  nia ya kufanya biashara hiyo aache mara moja.  

Mkurugenzi huyo alisisitiza kuwa Serikali imeweka jitihada kubwa ya kutoa elimu kwa watumiaji na waathirika wa dawa za kuelevya ili waweze kubadili tabia zao za kutumia dawa hizo na kuwa watu wema katika jamii. 

BAADHI YA KESI ZA DAWA ZA KULEVYA 
ZILIZOTOLEWA HUKUMU NA MAHAKAMA KUU 
NA WATUHUMIWA KUFUNGWA 

  1. Mwaka 2010 washitakiwa wanne walihukumiwa kifungo cha maisha jela Mahakama Kuu mkoani Mtwara baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na kilo nne za dawa za kulevya aina ya heroin. 

  2. Mwaka 2012 Mahakama Kuu Mkoani Tanga iliwahukumu washitakiwa 5 kifungo cha miaka 25 jela na kulipa faini ya TSh. 1,438,364,000/= kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kusafirisha kilo 92.2 za dawa za kulevya aina ya heroin. Pamoja na hukumu hiyo, mahakama iliamuru utaifishaji wa magari mawili yaliyotumiwa kusafirisha dawa hizo. 

  3. Mwaka 2012 Mahakama Kuu ilitoa hukumu ya miaka 20 jela kwa mshtakiwa mmoja aliyekamatwa na kilo 3 za dawa za kulevya aina ya heroin mkoani Kilimanjaro. 

MAHABUSU WENYE KESI ZA DAWA ZA KULEVYA 
GEREZA SEGEREA, WANAWAKE

Picture


Source: http://www.wavuti.com/4/post/2013/08/takwimu-za-serikali-za-mahabusu-wahukumiwa-wa-kesi-za-dawa-za-kulevya.html#ixzz2cWgb8G8n

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

Share this :

Related Posts

0 Comments