[wanabidii] WAZIRI JAFFO AONYA WATAKAOKWAMISHA JITIHADA ZA GREEN VOICES KUPAMBANA NA MAZINGIRA

Wednesday, July 19, 2017
CODES:
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<i><b><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Selemani Jaffo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi) akisikiliza maelezo kutoka kwa mama Abia Magembe kuhusu bidhaa zinazotokana na zao la muhogo. Kushoto kabisa ni Mratibu wa Mradi wa Green Voices kutoka Hispania, Alicia Cebada na kulia ni Mratibu wa mradi huo nchini Tanzania, Secelela Balisidya.</span></b></i></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">NAIBU Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(Tamisemi), Selemani Jaffo, amesema halmashauri zinawajibu wa kuunga mkono
jitihada za utunzaji wa mazingira na kupambana na mabadiliko ya tabianchi.</span></div>
<!--more--><o:p></o:p><br />
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Kutokana na hali hiyo, ameonya mtu yeyote asikwamishe
jitihada zinazofanywa na akinamama washiriki wa mradi wa Green Voices Tanzania
huku akiahidi kuwa serikali iko nao bega kwa bega.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Alisema kwamba, endapo kuna mtu katika idara zilizo chini ya
wizara yake atakwamisha jitihada zao, basi akinamama hao wawasiliane naye moja
kwa moja.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Akizungumza wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa
Green Voices nchini Tanzania uliofanyika kwenye Hoteli ya Golden Tulip jijini
Dar es Salaam, Naibu Waziri Jaffo alisema kwamba, wizara yake ndiyo yenye
jukumu kubwa la kuwawekea mazingira mazuri akinamama hao kutekeleza miradi yao
chini ya halmashauri husika, hivyo akawaahidi kuwapatia ushirikiano wa kutosha
kuhakikisha miradi hiyo inakuwa endelevu na suala la mazingira linapewa
kipaumbele.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Mradi wa Green Voices unatekelezwa katika mikoa ya Dar es
Salaam, Pwani, Morogoro, Kigoma, Mwanza na Kilimanjaro, kukiwa na miradi 10
ikiwemo ya kilimo cha mihogo, kilimo cha matunda, uyoga, ufugaji wa nyuki,
ukaushaji wa mbogamboga na utengenezaji wa majiko rafiki wa mazingira.<o:p></o:p></span></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<i><b><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Mratibu wa Mradi wa Green Voices kutoka Hispania, Alicia Cedaba (kushoto) akiwa na Leocadia Vedasto kutoka Ukerewe anayeratibu kilimo cha viazi lishe pamoja na usindikaji wa bidhaa zake. Katikati ni mdau mwingine aliyehudhuria uzinduzi wa awamu ya pili ya Mradi wa Green Voices Tanzania.</span></b></i></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<i><b><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Bidhaa za mbogamboga zilizokaushwa kutoka Morogoro.</span></b></i></div>
&nbsp;<span style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">Akinamama walioanzisha miradi hiyo – miradi na mikoa
watokayo vikiwa kwenye mabano –ni Regina Kamuli (Mkuranga, Pwani – </span><a href="https://www.jamiiforums.com/threads/dc-kihato-ni-aibu-mwanamke-kutoka-alfajiri-kutafuta-kuni-mume-amelala.1054634/" style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">Majiko
Banifu</a><span style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">), Abiah Magembe (Kisarawe, Pwani – </span><a href="http://www.fikrapevu.com/kilimo-cha-muhogo-chawanufaisha-akinamama-kisarawe/" style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">Usindikaji
wa Muhogo na Mtama</a><span style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">), Magdalena Bukuku (Kinondoni, Dar es Salaam – </span><a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/07/kilimo-cha-uyoga-dar-chawavutia.html" style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">Kilimo
cha Uyoga</a><span style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">), Mariam Bigambo (Dakawa, Morogoro – </span><a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/07/dakawa-green-voices-wafuga-nyuki.html" style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">Ufugaji
wa Nyuki</a><span style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">), na Esther Muffui (Morogoro – </span><a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/07/akinamama-morogoro-waelimishwa-jinsi-ya.html" style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">Ukaushaji
wa Mboga na Matunda</a><span style="font-family: Georgia, serif; font-size: 12pt;">).</span><br />
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Wengine ni Farida Makame (Kilimanjaro – <a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/12/mradi-wa-green-voices-wafanikisha.html">Majiko
ya Umeme-Jua</a>), Leocadia Vedastus (Ukerewe, Mwanza – <a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/07/dc-ukerewe-ashauri-wananchi-kulima.html">Kilimo
na Usindikaji wa Viazi Lishe</a>), Monica Kagya (Kisarawe, Pwani – <a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/07/wanawake-wafuga-nyuki-kuokoa-misitu-ya.html">Ufugaji
wa Nyuki</a>), Dkt. Sophia Mlote (Kinyerezi, Dar es Salaam – <a href="https://www.jamiiforums.com/threads/dk-mlote-kilimo-hifadhi-kitanikomboa-hata-nikistaafu.1048022/">Kilimo
Hai cha Nyanya na Mbogamboga</a>), na Evelyn Kahembe (Uvinza, Kigoma – Kilimo
cha Matunda).<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Kupitia miradi hiyo, zaidi ya wanawake 300 wamepatiwa
mafunzo mbalimbali huku program nyingine za mafunzo kwa vitendo zikiendelea
katika makundi yao.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">&nbsp;"Serikali ya Tanzania
na hasa wizara hii, na wizara hii Mheshimiwa Rais mwenyewe ni wizara yake,
naomba niwahakikishie kwamba tutashirikiana na Green Voices kwa nguvu zote na nitawapa
pasiwedi ya kuwasiliana na ofisi yangu moja kwa moja ili kama mnakwama mambo
yenu yaweze kwenda huko katika halmashauri mlipo," alisema Jaffo, ambaye pia ni
Mbunge wa Jimbo la Kisarawe mkoani Pwani. <o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Akaongeza: "Nitawaunganisha na mkurugenzi maalum wa idara za
serikali katika wizara yangu, kwamba ninyi mkikwama katika halmashauri kwa jambo
lolote lile mnawasiliana naye &nbsp;moja kwa
moja mradi mambo yenu yaweze kwenda mpate sapoti, sauti ya wanawake iweze
kusikika, mambo ya mazingira yaweze kubadilika, kilimo, mifugo na kadhalika ili
mwisho wa siku watu waseme kwamba kuna kundi la watu walikwenda Hispania na
wakajifunza wakaleta mabadiliko nchini."<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Aidha, Naibu Waziri Jaffo alisema kundi hilo la akinamama wa
Green Voices ni muhimu na serikali itahakikisha inawaunga mkono kwa kila hali.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">"Ninyi ni kioo cha jamii na watu wengi wanatakiwa
wajifunze kutoka kwenu. Kumbukeni, katika suala la mazingira maeneo mengi
yameathirika sana, mnaweza kuona jinsi maeneo mengi yanavyokumbwa na mafuriko
kutokana na watu kukata miti na kuharibu mazingira, wakati mwingine
tunashuhudia ukame wa kutisha. <o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">"Kwahiyo ninyi mradi wenu unakwenda kukabiliana na
changamoto hizi, ni muhimu sana, mna wajibu mkubwa sana kwa sababu suala la
mazingira ni muhimu na linaathiri dunia. <o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">"Tunatakiwa tutoke katika miradi isiyo halisi (<i>artificial projects</i>) na kwenda kwenye miradi
halisi ili tuweze kubadilisha maisha ya watu." <o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Vile vile, aliwaasa akinamama hao kwamba, wakienda huko waongee
lugha rahisi na wananchi ili iwe rahisi kueleweka. <o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">"Ninyi hapa wote ni wasomi, lakini mkienda huko ongeeni
lugha rahisi ili mwananchi wakawaida akisikia aweze kuielewa na kuleta
mabadiliko ya kweli. Mama mwingine hajasoma hata darasa moja na inawezekana
kuwepo kwako wewe kukabadili maisha yake," alisema.</span></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<i><b>Naibu Waziri wa Tamisemi, Selemani Jaffo, akizungumza katika uzinduzi huo.</b></i>&nbsp;&nbsp;</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<i><b><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Secelela Balisidya akipokea cheti.</span></b></i></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Mmoja wa washiriki wa mradi wa Green Voices, Mariam Bigambo,
mkulima wa Mvomero ambaye amejikita katika ufugaji wa nyuki akiwa na kikundi
cha wanawake 15, alisema kwamba licha ya umuhimu wa mradi huo, lakini
wanakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinakwamisha maendeleo yao.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">"Changamoto kubwa tunayokabiliana nayo ni kushushwa kwa
mizinga yetu na watu wasiojulikana kwa sababu tumeiweka porini," alisema na
kuongeza: "Kila mara tunakuta mizinga yetu imeshushwa, tumekwishatoa taarifa
kwa serikali ya kijiji pamoja na kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Mvomero na hata Polisi."<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Aidha, alisema kwamba, ufugaji wa nyuki unahitaji uvumilivu
na mpaka sasa baadhi ya wanakikundi wamevunjika moyo kwa sababu bado
hawajanufaika na matunda ya kazi yao.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Kutokana na hali hiyo, alisema, wameamua pia kugeukia kilimo
cha uyoga ili kuongeza tija.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Mratibu wa mradi wa Green Voices nchini Tanzania, Secelela
Balisidya, alisema awamu ya kwanza ya mradi huo ililenga katika uanzishwaji na
uzalishaji, lakini awamu ya pili inalenga kuwapatia stadi akinamama ili
kuboresha bidhaa wanazozizalisha ili ziongezeke ubora la kuwaletea tija.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">"Hivi sasa katika awamu ya pili akinamama watapatiwa mafunzo
ya namna ya kutengeneza bidhaa zao kama vifungashio ili kuongeza ubora na
thamani na tunataka bidhaa zao ziingie sokoni katika viwango ambavyo
vinakubalika," alisisitiza.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Akizungumza katika uzinduzi huo wa awamu ya pili, Mratibu wa
mradi wa Green Voices kutoka Hispania kutoka taasisi ya Women for Africa
Foundation inayodhamini mradi huo, Alicia Cebada, <a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/10/wafadhili-mradi-wa-green-voices.html">alisema
wamefarijika na mradi huo kwa kuwa umeonyesha mafanikio makubwa nchini Tanzania</a>
katika awamu ya kwanza na ndiyo maana wameamua kuwaongezea uwezo akinamama hao
katika awamu hii.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">&nbsp;"Tumekuwa
tukiwasiliana mara kwa mara na Secelela (Mratibu wa Green Voices Tanzania)
kuhusu mafanikio na changamoto za mradi huu na kwa kweli tunafarijika kuona
miradi yote inakwenda vizuri," alisema Alicia.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Alisema, changamoto pekee ambayo ipo mbele yao ni
kuhakikisha miradi hiyo inasimama na kuwafundisha wanawake wengi kadiri wawezavyo
ili kuhakikisha wanajiletea maendeleo katika maeneo yao kiuchumi na kijamii.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Mwaka 2016 rais wa mfuko wa Women for Africa Foundation,
Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, alizuru nchini Tanzania na kushiriki
uzinduzi wa mradi huo Julai 11, 2016 ambapo ulizinduliwa rasmi na Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Katika uzinduzi huo, Mama Samia aliahidi kwamba serikali
yake itahakikisha inakuwa bega kwa bega kusaidia miradi hiyo iwe endelevu ili
kuunga mkono juhudi za utunzaji wa mazingira na kupambana na mabadiliko ya
tabianchi, kuongeza uhakika wa chakula, kuwakwamua wananchi na umaskini pamoja
na kuongeza ajira, hasa kwa wanawake.<o:p></o:p></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: &quot;Georgia&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-size: 11.0pt;">Kwa upande wake, Mama Maria Tereza, ambaye ni makamu wa rais
mstaafu wa Hispania, alieleza kufurahishwa kwake na jitihada za akinamama wa
Tanzania na kusema taasisi yake inaangalia namna ya kuwasaidia zaidi.<o:p></o:p></span></div>
<br />
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<br /></div>


​KAWAIDA:

Selemani Jaffo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi) akisikiliza maelezo kutoka kwa mama Abia Magembe kuhusu bidhaa zinazotokana na zao la muhogo. Kushoto kabisa ni Mratibu wa Mradi wa Green Voices kutoka Hispania, Alicia Cebada na kulia ni Mratibu wa mradi huo nchini Tanzania, Secelela Balisidya.

 

NAIBU Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jaffo, amesema halmashauri zinawajibu wa kuunga mkono jitihada za utunzaji wa mazingira na kupambana na mabadiliko ya tabianchi.


Kutokana na hali hiyo, ameonya mtu yeyote asikwamishe jitihada zinazofanywa na akinamama washiriki wa mradi wa Green Voices Tanzania huku akiahidi kuwa serikali iko nao bega kwa bega.

Alisema kwamba, endapo kuna mtu katika idara zilizo chini ya wizara yake atakwamisha jitihada zao, basi akinamama hao wawasiliane naye moja kwa moja.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa Green Voices nchini Tanzania uliofanyika kwenye Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri Jaffo alisema kwamba, wizara yake ndiyo yenye jukumu kubwa la kuwawekea mazingira mazuri akinamama hao kutekeleza miradi yao chini ya halmashauri husika, hivyo akawaahidi kuwapatia ushirikiano wa kutosha kuhakikisha miradi hiyo inakuwa endelevu na suala la mazingira linapewa kipaumbele.

Mradi wa Green Voices unatekelezwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Kigoma, Mwanza na Kilimanjaro, kukiwa na miradi 10 ikiwemo ya kilimo cha mihogo, kilimo cha matunda, uyoga, ufugaji wa nyuki, ukaushaji wa mbogamboga na utengenezaji wa majiko rafiki wa mazingira.

Mratibu wa Mradi wa Green Voices kutoka Hispania, Alicia Cedaba (kushoto) akiwa na Leocadia Vedasto kutoka Ukerewe anayeratibu kilimo cha viazi lishe pamoja na usindikaji wa bidhaa zake. Katikati ni mdau mwingine aliyehudhuria uzinduzi wa awamu ya pili ya Mradi wa Green Voices Tanzania.

Bidhaa za mbogamboga zilizokaushwa kutoka Morogoro.

 Akinamama walioanzisha miradi hiyo – miradi na mikoa watokayo vikiwa kwenye mabano –ni Regina Kamuli (Mkuranga, Pwani – Majiko Banifu), Abiah Magembe (Kisarawe, Pwani – Usindikaji wa Muhogo na Mtama), Magdalena Bukuku (Kinondoni, Dar es Salaam – Kilimo cha Uyoga), Mariam Bigambo (Dakawa, Morogoro – Ufugaji wa Nyuki), na Esther Muffui (Morogoro – Ukaushaji wa Mboga na Matunda).

Wengine ni Farida Makame (Kilimanjaro – Majiko ya Umeme-Jua), Leocadia Vedastus (Ukerewe, Mwanza – Kilimo na Usindikaji wa Viazi Lishe), Monica Kagya (Kisarawe, Pwani – Ufugaji wa Nyuki), Dkt. Sophia Mlote (Kinyerezi, Dar es Salaam – Kilimo Hai cha Nyanya na Mbogamboga), na Evelyn Kahembe (Uvinza, Kigoma – Kilimo cha Matunda).

Kupitia miradi hiyo, zaidi ya wanawake 300 wamepatiwa mafunzo mbalimbali huku program nyingine za mafunzo kwa vitendo zikiendelea katika makundi yao.

 "Serikali ya Tanzania na hasa wizara hii, na wizara hii Mheshimiwa Rais mwenyewe ni wizara yake, naomba niwahakikishie kwamba tutashirikiana na Green Voices kwa nguvu zote na nitawapa pasiwedi ya kuwasiliana na ofisi yangu moja kwa moja ili kama mnakwama mambo yenu yaweze kwenda huko katika halmashauri mlipo," alisema Jaffo, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisarawe mkoani Pwani.

Akaongeza: "Nitawaunganisha na mkurugenzi maalum wa idara za serikali katika wizara yangu, kwamba ninyi mkikwama katika halmashauri kwa jambo lolote lile mnawasiliana naye  moja kwa moja mradi mambo yenu yaweze kwenda mpate sapoti, sauti ya wanawake iweze kusikika, mambo ya mazingira yaweze kubadilika, kilimo, mifugo na kadhalika ili mwisho wa siku watu waseme kwamba kuna kundi la watu walikwenda Hispania na wakajifunza wakaleta mabadiliko nchini."

Aidha, Naibu Waziri Jaffo alisema kundi hilo la akinamama wa Green Voices ni muhimu na serikali itahakikisha inawaunga mkono kwa kila hali.

"Ninyi ni kioo cha jamii na watu wengi wanatakiwa wajifunze kutoka kwenu. Kumbukeni, katika suala la mazingira maeneo mengi yameathirika sana, mnaweza kuona jinsi maeneo mengi yanavyokumbwa na mafuriko kutokana na watu kukata miti na kuharibu mazingira, wakati mwingine tunashuhudia ukame wa kutisha.

"Kwahiyo ninyi mradi wenu unakwenda kukabiliana na changamoto hizi, ni muhimu sana, mna wajibu mkubwa sana kwa sababu suala la mazingira ni muhimu na linaathiri dunia.

"Tunatakiwa tutoke katika miradi isiyo halisi (artificial projects) na kwenda kwenye miradi halisi ili tuweze kubadilisha maisha ya watu."

Vile vile, aliwaasa akinamama hao kwamba, wakienda huko waongee lugha rahisi na wananchi ili iwe rahisi kueleweka.

"Ninyi hapa wote ni wasomi, lakini mkienda huko ongeeni lugha rahisi ili mwananchi wakawaida akisikia aweze kuielewa na kuleta mabadiliko ya kweli. Mama mwingine hajasoma hata darasa moja na inawezekana kuwepo kwako wewe kukabadili maisha yake," alisema.

Naibu Waziri wa Tamisemi, Selemani Jaffo, akizungumza katika uzinduzi huo.  

Secelela Balisidya akipokea cheti.

Mmoja wa washiriki wa mradi wa Green Voices, Mariam Bigambo, mkulima wa Mvomero ambaye amejikita katika ufugaji wa nyuki akiwa na kikundi cha wanawake 15, alisema kwamba licha ya umuhimu wa mradi huo, lakini wanakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinakwamisha maendeleo yao.

"Changamoto kubwa tunayokabiliana nayo ni kushushwa kwa mizinga yetu na watu wasiojulikana kwa sababu tumeiweka porini," alisema na kuongeza: "Kila mara tunakuta mizinga yetu imeshushwa, tumekwishatoa taarifa kwa serikali ya kijiji pamoja na kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero na hata Polisi."

Aidha, alisema kwamba, ufugaji wa nyuki unahitaji uvumilivu na mpaka sasa baadhi ya wanakikundi wamevunjika moyo kwa sababu bado hawajanufaika na matunda ya kazi yao.

Kutokana na hali hiyo, alisema, wameamua pia kugeukia kilimo cha uyoga ili kuongeza tija.

Mratibu wa mradi wa Green Voices nchini Tanzania, Secelela Balisidya, alisema awamu ya kwanza ya mradi huo ililenga katika uanzishwaji na uzalishaji, lakini awamu ya pili inalenga kuwapatia stadi akinamama ili kuboresha bidhaa wanazozizalisha ili ziongezeke ubora la kuwaletea tija.

"Hivi sasa katika awamu ya pili akinamama watapatiwa mafunzo ya namna ya kutengeneza bidhaa zao kama vifungashio ili kuongeza ubora na thamani na tunataka bidhaa zao ziingie sokoni katika viwango ambavyo vinakubalika," alisisitiza.

Akizungumza katika uzinduzi huo wa awamu ya pili, Mratibu wa mradi wa Green Voices kutoka Hispania kutoka taasisi ya Women for Africa Foundation inayodhamini mradi huo, Alicia Cebada, alisema wamefarijika na mradi huo kwa kuwa umeonyesha mafanikio makubwa nchini Tanzania katika awamu ya kwanza na ndiyo maana wameamua kuwaongezea uwezo akinamama hao katika awamu hii.

 "Tumekuwa tukiwasiliana mara kwa mara na Secelela (Mratibu wa Green Voices Tanzania) kuhusu mafanikio na changamoto za mradi huu na kwa kweli tunafarijika kuona miradi yote inakwenda vizuri," alisema Alicia.

Alisema, changamoto pekee ambayo ipo mbele yao ni kuhakikisha miradi hiyo inasimama na kuwafundisha wanawake wengi kadiri wawezavyo ili kuhakikisha wanajiletea maendeleo katika maeneo yao kiuchumi na kijamii.

Mwaka 2016 rais wa mfuko wa Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, alizuru nchini Tanzania na kushiriki uzinduzi wa mradi huo Julai 11, 2016 ambapo ulizinduliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan.

Katika uzinduzi huo, Mama Samia aliahidi kwamba serikali yake itahakikisha inakuwa bega kwa bega kusaidia miradi hiyo iwe endelevu ili kuunga mkono juhudi za utunzaji wa mazingira na kupambana na mabadiliko ya tabianchi, kuongeza uhakika wa chakula, kuwakwamua wananchi na umaskini pamoja na kuongeza ajira, hasa kwa wanawake.

Kwa upande wake, Mama Maria Tereza, ambaye ni makamu wa rais mstaafu wa Hispania, alieleza kufurahishwa kwake na jitihada za akinamama wa Tanzania na kusema taasisi yake inaangalia namna ya kuwasaidia zaidi.

 


--
Brother Danny Blog (Kisima cha Hekima na Busara)
Cell: +255 - 715 - 070 109
Whatsapp: +255 - 656 - 331 974

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Previous
Next Post »
0 Comments