Lowassa kashaibadilisha Chadema.
1. Kabadilisha ratiba yao ya uchaguzi.
2. Kabadilisha mgombea wao. Dr. Slaa anakatwa kwa sababu ya Lowassa.
3. Kabadilisha bajeti yao ya uchaguzi.
4. Kabadilisha kauli zao kuhusu ufisadi.
5. Kabadilisha ilani yao ya uchaguzi.
Sasa tujiulize, nani anayebadili mwenzie? Chadema itambadili Lowassa au Lowassa anaibadili Chadema?
Lowassa yuko kwenye siasa muda mrefu kuliko umri wa Chadema. Kuamini kuwa Lowassa atabadilika ghafla ni kujidanganya kulikopitiliza.
Mpaka sasa Chadema haijabadili chochote kwa Lowassa, yeye ndio anawabadili.
Chadema badala ya kuleta mabadiliko, yenyewe ndio inabadilishwa...
Related Posts
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Comments