CCM oyeee,wakina mama,wazee tungurume kama Simba.
- Sasa tutulie tusikie neno kubwa.(Anamshukuru Mungu.)
-Nichukue nafasi hii kwa niaba ya familia yangu kuwashukuru kwa kufika kwenu hapa.
-Jogoo litakapopambanishwa na wapinzani mwezi Oktoba.
- Anatambulisha wageni waalikwa waliofika na kuwashukuru,anawashukuru wanajimbo la Mtama kwa kumuamini kwa miaka 15 kuwaongoza katika ngazi ya ubunge.
- Jimbo la Mtama liko salama na litaendelea kuongozwa na CCM hata kama nikiondoka,hakuna cha UKAWA wala UKIWA kuongoza jimbo salama la CCM.
- Nimesimama mbele yenu kutia nia kuwania nafasi ya juu ambayo ni ya Urais.
- Nimejipima,nimetuma watu wangu nchini kufanya tathmini,nimeridhika.Nina uzoefu kwenye chama,serikalini na kimataifa hivyo nimeona nafaa,nafaa kushika nafasi kubwa nchini,nafasi ya urais.
- Nimeingia kwnye chama nikiwa na miaka 22 nimemkuta mwalimu Mangula,Amenifundisha siasa.Pia kwenye chama nimeshika nafasi mbalimbali za kiuongozi kuanzia ngazi ya chini mpaka za juu (Anazitaja) - Nani kama Membe? Wananchi... Hakuna. (Anaendelea...
- Pia katika upande wa serikali hii,Nimepata uzoefu. 1978 nimekuwa kwenye idara ya usalama wa taifa.Nimefanya kazi kwenye Ubalozi kuanzia 1992 mpaka 2000 huko Canada.
- Nimekuwa naibu Waziri (Anantaja wizara husika mbili)
- Nimekuwa waziri wa Mambo ya Njee na ushirikiano wa kimataifa kwa muda mrefu.
- Anataja uzoefu wake nje ya mipika ya Tanzania (Kimataifa)
- Uzoefu huu na elimu ya kutosha vinakidhi vigezo vilivyoweka na CCM ili kuwa mgombea wa Urais.Hata vikiongezwa vingine basi tutavitimiza. Nani kama Membe...Hakuna.
- Nimetafakari sana kuhusu Urais nimeona niombe,Nimejilinganisha na watu wengine wote watia nia, na baada ya kumpitia mmoja baada ya mwingine nimeona Lindi tuna nafasi ya Kuchukua na kuwa na kiongozi wa juu Tanzania.
- Kuna nafasi za kukurupuka kuchukua lakini sio hii ya Urais, hii nafasi Muachie Membe ndio anafaa.
- Mwezi Machi mwaka huu nilikwenda Butiama kwenye sherehe za wazanaki,Nilialikwa na Chifu wa wazanaki (Wanzagi), Sikutaka kupoeza hiyo nafasi nilikimbilia haraka ili pia nikazulu kaburi la Baba wa Taifa.
- Nilisali sana kwenye kaburi la baba wa Taifa. Nilimuomba kuhusu kutia nia yangu ya kugombea Urais,kuna viatu ulivyovyiacha alivaa Mzee Mwinyi,Mzee Mkapa na Kikwete,wote hawa viliwatosha. Sasa naomba uniachie mimi nivivae.
- Pia nilimwambia mwalimu kama unaona hivi viatu havinitoshi,wewe na Mungu nipitishieni Mbali kikombe hichi.Lakini timu yangu niliyokuwa nayo iliniambia niombe,nikajiuliza mwalimu Nyerere kanisikiliza.
- Nimemtaja Mwalimu Nyerere kwasababu yeye ndio baba wa Taifa na aliyetuletea uhuru.
- Kiongozi unajisikia raha gani kuingia Ikulu kwa kununua Urais,tununue vyeo vingine lakini sio Ikulu.Ikulu hainunuliki.
- Mkapa alivyoingia alifungua barabara hasa huku Lindi na Mtwara sasa panapitika.
- Alivyoingia Kikwete aliendeleza pale na kufungua milango ya elimu. Kikwete ametoa mchango mkubwa wa kuendeleza elimu kuliko Marais waliomtangulia.
- Nikichaguliwa kuwa Rais nataka watoto wetu wawe wenye afya na wapate elimu,wamama wasitembee umbali mrefu kufuata zahanati.Madawa yawepo ya kutosha kwenye zahanati.
- Nina mambo mawili ambayo ningependa kuyasema, moja ni kuichukua Tanzania kuelekea kwenye uchumi wa viwanda ulioegemea kwenye kilimo.
- Gesi iliyogunduliwa hapo pale ili kulete mwanga tu bali kuleta uchumi wa viwanda.Tunataka viwanda vitakavyo ajiri vijana.
- Pili kuuza malighafi zinazozalishwa viwandani.Tumechoka kuuziwa bidhaa kutoka jirani zetu.Yaani maligafi tuzalishe huku,wenyewe wachukue wakasindike alafu waje huku kutuuzia.Tunahitaji viwanda vyetu wenyewe ambavyo vitakuwa vinazalisha bidhaa.
Utawala Bora,
Nianze ulinzi na usalama.Nchi yetu ina tatizo la kuuawa albino,madawa ya kulevya,ujambazi na vitisho.Breki ya matukio haya unaisha mwezi wa saba.Nitapambana na kutokomeza mabo yote yanayoathiria usalama wa taifa letu na wala sitotetereka.
-Nitaimarisha vyombo vya usalama kwenye miji mikubwa na midogo.Nchi hii ilikuwa ya amani na itaendelea kuwa ya amani.
Muungano:
- Tanganyika na Zanzibar.Muungano wetu ni wa kipekee duniani,hakuna sehemu nchi nyingine muungano uliodumu kama huu wetu.Hii ni TUNU aliyotuachia baba wa Taifa.Nikichaguliwa nitaulinda huu Muungano na hakuna wa kuuvunja.
-Mapinduzi Zanzibar - Kuna watu wanakebehi Mapinduzi ya Zanzibar,hawajui kuwa mapinduzi yale yalimuweka huru mtu mweusi.Nikichaguliwa nitayazingatia Mapinduzi ya Zanzibar
Sekta binafsi
- Nchi yetu lazma isukumwe kimaendeleo na sekta binafsi. Hatujaweza kushirikiana na sekta binafsi ili kukuza uchumi na kuleta ajira. Hatujaunganisha sekta binafsi na sekta za umma ili kuleta maendeleo.Nikichaguliwa nitaunganisha na kuletea umoja ili ushirikiano ule uweze kukuza uchumi.
- Nikichaguliwa kuwa Rais lazma nihakikishe wakina baba wanawaheshimu wakina mama.Wakina baba muache ulevi,muache kulewa na kuwaonea wakina mama.
ELIMU:
Nikichaguliwa mkazo mkubwa utakuwa kwenye shule za Ufundi na VETA.Tutafufua vyote hivi maana ndio vinaongoza kwa kutoa ajaira.Hata kwenye viwanda wanahitaji wenye ujuzi ambao wengi wanazalishwa na vyuo hivi vya ufundi.
Michezo na sanaa;
Nikichaguliwa nitafanya
- Nitasimamia kuondoa zana kuwa Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu kuwa tunakuwa wa mwisho kwenye michezo
- Tutafungua vyuo vya michezo mbalimbali na kuwaandaa wanamichezo.
Maigizo; Tutahakikisha kuwa tunawasimamia ili mpate haki zenu za msingi kama Hatimiliki,tatutawalinda kwa nguvu zote.
UTAWALA BORA: Nikichaguliwa nitasimamia....
1.Rushwa: Anayetoa rushwa ana makosa na anayepokea ana makosa, tutakibadilisha hiki kifungu na kumbana yule Anayepokea,aliyeomba(Anatoa mifano Scenario)
- Anawaasa watu kuwa waweze kutoa taarifa za rushwa kuliko kukaa kimya huku mambo yakiharibika.Anawaambia waandishi wa habari kufichua mianya ya rushwa kutoa taarifa na kuiachia polisi kufanya kazi yake.
-Anasema hatafumbia macho mla rushwa,lazma nchi hii tuiweke kwenye mstari wa mwalimu Nyerere,Mwinyi, Mkapa na Kikwete.Lazma tuiweke kwenye misingi bora. Anasema wafanyabiashara wanaokwepa kulipa kodi watalipa tu hizo kodi.Nichague mimi ili niweze kusimamia serikali yenye uadilifu.
* Anamalizia kwa kuwashukuru wa kumsikiliza.
Naweka nia kugombea Urais awamu ya tano.Chama cha CCM kina marafiki wengi sana njee ya mipaka ya Tanzania( Anataja Vyama rafiki vya CCM duniani.) Lazma chama tukijenge,lazma chama chetu kichaguliwe mwaka 2015.
*Anawaonea huruma wenzao (Upinzani) kuwa tokea mfumo wa vyama vingi hawajawahi kushinda urais.
-Anawashangaa kuwa kila uchaguzi wanaweka mgombea yule yule ambaye anakuwa kama mfalme pamoja nauongozi wake kushindwa urais mara kwa mara.
- Kila uchaguzi wanasingizia kuibiwa kura.
- Anasema kuwa wale wafalme hawataki kuachia ngazi na kubadilisha uongozi wa kifalme( Anaelezea sokosoko utakalopata kama ukitaka kugombea nafasi ya juu na kuitwa msaliti mamluki).
- Anasema uongozi ule ule unaoshindwa miaka yote hawawezi kushinda,watachapwa asubuhi mapema.
- Anasema kuwa wao wanabadilisha Magamba kuanzia kwa Mwalimu Nyerere,Mzee Mwingi,Mzee Mkapa na mpaka sasa Rais Kikwete. Hivyo lazma waendelee kushinda.
-Nchi hii itakuwa salama endapo Chama cha Mapinduzi kitaendelea kuwa madarakani.Tunahitaji Rais muadilifu,mwenye nia ya dhati,mwenye maono.
- Naomba mnisindikize kwenye jengo kubwa,jeupe,jengo la Ikulu ili twende tukamalizie ambapo pale mzee Kikwete ameishia.
Anamalizia kwa kuimba nyimbo ya Kimwera.
Sr. Kahama, Hadija Jabir,wabunge wa Lindi na Mtwara na wabunge wengine marafiki,w/kiti wa Pwani,Lindi Naibu Waziri wa mifugo na uvuvi,Viongozi wa dini mbalimbali walifuatana na Membe wakati wa kutangaza nia yake
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments