TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
HABARI YA UPOTOSHWAJI ILIYOANDIKWA NA GAZETI LA NIPASHE KUNIHUSISHA NA KASHFA YA MABEHEWA FEKI YA TRL
JOTO la uchaguzi mkuu limezidi kupanda baada ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe kusema tuhuma zinazotolewa dhidi yake ni porojo na uzushi kuelekea kipindi hiki cha uchaguzi. Mwakyembe alisema baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika kuhusu mabehewa ya TRL na kumhusisha yeye wakati alikwisha agiza hatua za kuchukuliwa kwa wahusika tangu waziri wa uchukuzi.
Imeandika habari yenye kichwa cha habari "Mwakyembe atajwa Kashfa ya TRL". Napenda kutoa ufafanuzi kuwa habari hiyo iliyoandikwa ni uzushi mtupu wa kutaka kunichafua. Nachelea kusema habari hii ni uzushi na porojo za kisiasa haswa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kwa kunihusisha kwenye mchakato wa zabuni ya TRL ambao Waziri hana mamlaka nao kikanuni na kisheria.
Kama Waziri mwenye dhamana na Wizara baada ya kupokea malalamiko kuhusu mabehewa yaliyonunuliwa na TRL kutokuwa na viwango vinavyokubalika, nilichukua hatua za awali za kuunda tume ambayo ilanza mara moja kuchunguza suala hili ili kujiridhisha na kutafuta ukweli wa jambo hilo. Baada ya kupokea taarifa ya awali ya uchunguzi uliofanywa na tume hiyo, nilichukua uamuzi wa kuiagiza Bodi ya Wakurugenzi ya TRL kuivunja Bodi ya Zabuni.
Baada ya bodi hiyo zabuni kuvunjwa, niliagiza Bodi ya Wakurugenzi ya TRL iwasimamishe kazi maafisa waandamizi wote wa TRL waliohusika katika mchakato wa manunuzi wa mabehewa hayo ili kupisha uchunguzi uliokuwa ukiendelea kufanywa na tume. Aidha, niliiagiza Wizara na Bodi ya Wakurugenzi ya TRL kuiomba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)ifanye uchunguzi wa kina wa mkasa mzima, kazi ambayo nafahamu inaendelea kufanyika hadi sasa.
Kwa msingi huo habari iliyoandikwa kwenye gazeti hilo (NIPASHE) vyombo hivyo (si hili) ya kunihusisha na kashfa ya sakata hilo imenishtua na kunishangaza kwa kuwa kama ningekuwa nahusika kwa namna moja au nyingine nisingeweza kuchukua hatua nilizozieleza hapo juu. Gazeti la NIPASHE pia limehusisha suala la mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yalyofanywa na Mhe. Rais, ambayo mimi nimehamishiwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwamba ni kwa sababu ya kuniepusha na kadhia ya kashfa hiyo ya ununuzi wa mabehewa feki.
Hilo ni jambo la kushangaza na uelewa mdogo wa mwandishi wa kutoelewa namna Serikali inavyofanya kazi. Uamuzi wa kunihamisha Wizara umefanywa na Rais kwa sababu tofauti kabisa na hizo za kusadikika zilizoandikwa na gazeti la NIPASHE. Kama Rais aliona nina dosari, hakuwa na sababu kabisa kuniteua kumsaidia kuendesha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika kipindi hiki ambacho nchi yetu imepata fursa ya kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya. Hivi karibuni Mhe.
Waziri Mkuu, alifanya ziara katika Mkoa wa Mbeya na wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Kyela, Waziri Mkuu alitoa ufanunuzi mzuri wa uamuzi uliochukuliwa na Mhe. Rais wa kuniamisha kutoka Wizara ya Uchukuzi kwenda Wizara ya Ushirikano wa Afrika Mashariki, maelezo ambayo sina haja ya kurudia kuyaeleza kwa sababu yalishatolewa kwenye vyombo vya habari.
Nimalizie kwa kusema kuwa Watanzania tuamke kwani hakuna dosari yoyote ya mimi kuhamishiwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kupelekwa kwangu Afrika ya Mashariki ambako nilianzia Ubunge, ni mkakati mzuri tu wenye tija. Wenye nia njema na nchi yetu wataafiki". Naomba ifahamike kwamba sehemu kubwa ya nguvu ya fedha ya washiriki wetu wa maendeleo sasa inapitia kwenye Jumuiya za kanda kama Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo kwa sasa Mhe. Rais ni Mwenyekiti wa Marais wa Jumuiya na mimi ni Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri.
Hivi sasa niko njiani natokea Marekani ambako niliongoza ujumbe mkubwa wa Mawaziri wan nchi tano (5) za Jumuiya ya Afrika Mashariki kujadiliana na Serikali ya Marekani, pamoja na mambo mengine, kuongeza muda wa sheria inayozipa fursa nchi za EAC kupeleka bidhaa za biashara Marekani bila ushuru (AGOA).
Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb)
WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
9 Machi, 2015
-- WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
HABARI YA UPOTOSHWAJI ILIYOANDIKWA NA GAZETI LA NIPASHE KUNIHUSISHA NA KASHFA YA MABEHEWA FEKI YA TRL
JOTO la uchaguzi mkuu limezidi kupanda baada ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe kusema tuhuma zinazotolewa dhidi yake ni porojo na uzushi kuelekea kipindi hiki cha uchaguzi. Mwakyembe alisema baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika kuhusu mabehewa ya TRL na kumhusisha yeye wakati alikwisha agiza hatua za kuchukuliwa kwa wahusika tangu waziri wa uchukuzi.
Imeandika habari yenye kichwa cha habari "Mwakyembe atajwa Kashfa ya TRL". Napenda kutoa ufafanuzi kuwa habari hiyo iliyoandikwa ni uzushi mtupu wa kutaka kunichafua. Nachelea kusema habari hii ni uzushi na porojo za kisiasa haswa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kwa kunihusisha kwenye mchakato wa zabuni ya TRL ambao Waziri hana mamlaka nao kikanuni na kisheria.
Kama Waziri mwenye dhamana na Wizara baada ya kupokea malalamiko kuhusu mabehewa yaliyonunuliwa na TRL kutokuwa na viwango vinavyokubalika, nilichukua hatua za awali za kuunda tume ambayo ilanza mara moja kuchunguza suala hili ili kujiridhisha na kutafuta ukweli wa jambo hilo. Baada ya kupokea taarifa ya awali ya uchunguzi uliofanywa na tume hiyo, nilichukua uamuzi wa kuiagiza Bodi ya Wakurugenzi ya TRL kuivunja Bodi ya Zabuni.
Baada ya bodi hiyo zabuni kuvunjwa, niliagiza Bodi ya Wakurugenzi ya TRL iwasimamishe kazi maafisa waandamizi wote wa TRL waliohusika katika mchakato wa manunuzi wa mabehewa hayo ili kupisha uchunguzi uliokuwa ukiendelea kufanywa na tume. Aidha, niliiagiza Wizara na Bodi ya Wakurugenzi ya TRL kuiomba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)ifanye uchunguzi wa kina wa mkasa mzima, kazi ambayo nafahamu inaendelea kufanyika hadi sasa.
Kwa msingi huo habari iliyoandikwa kwenye gazeti hilo (NIPASHE) vyombo hivyo (si hili) ya kunihusisha na kashfa ya sakata hilo imenishtua na kunishangaza kwa kuwa kama ningekuwa nahusika kwa namna moja au nyingine nisingeweza kuchukua hatua nilizozieleza hapo juu. Gazeti la NIPASHE pia limehusisha suala la mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yalyofanywa na Mhe. Rais, ambayo mimi nimehamishiwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwamba ni kwa sababu ya kuniepusha na kadhia ya kashfa hiyo ya ununuzi wa mabehewa feki.
Hilo ni jambo la kushangaza na uelewa mdogo wa mwandishi wa kutoelewa namna Serikali inavyofanya kazi. Uamuzi wa kunihamisha Wizara umefanywa na Rais kwa sababu tofauti kabisa na hizo za kusadikika zilizoandikwa na gazeti la NIPASHE. Kama Rais aliona nina dosari, hakuwa na sababu kabisa kuniteua kumsaidia kuendesha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika kipindi hiki ambacho nchi yetu imepata fursa ya kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya. Hivi karibuni Mhe.
Waziri Mkuu, alifanya ziara katika Mkoa wa Mbeya na wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Kyela, Waziri Mkuu alitoa ufanunuzi mzuri wa uamuzi uliochukuliwa na Mhe. Rais wa kuniamisha kutoka Wizara ya Uchukuzi kwenda Wizara ya Ushirikano wa Afrika Mashariki, maelezo ambayo sina haja ya kurudia kuyaeleza kwa sababu yalishatolewa kwenye vyombo vya habari.
Nimalizie kwa kusema kuwa Watanzania tuamke kwani hakuna dosari yoyote ya mimi kuhamishiwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kupelekwa kwangu Afrika ya Mashariki ambako nilianzia Ubunge, ni mkakati mzuri tu wenye tija. Wenye nia njema na nchi yetu wataafiki". Naomba ifahamike kwamba sehemu kubwa ya nguvu ya fedha ya washiriki wetu wa maendeleo sasa inapitia kwenye Jumuiya za kanda kama Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo kwa sasa Mhe. Rais ni Mwenyekiti wa Marais wa Jumuiya na mimi ni Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri.
Hivi sasa niko njiani natokea Marekani ambako niliongoza ujumbe mkubwa wa Mawaziri wan nchi tano (5) za Jumuiya ya Afrika Mashariki kujadiliana na Serikali ya Marekani, pamoja na mambo mengine, kuongeza muda wa sheria inayozipa fursa nchi za EAC kupeleka bidhaa za biashara Marekani bila ushuru (AGOA).
Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb)
WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
9 Machi, 2015
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments