[wanabidii] Watanzania Wa Vijijini Watamkumbuka JK Kama ' Rais Wa Umeme'

Friday, January 09, 2015


Ndugu zangu,

Ama hakika, Watanzania wa Vijijini watamkumbuka Rais Jakaya Kikwete kama ' Rais wa Umeme'.

Jana nilifika kijijini kwetu Nyeregete, Mbarali, Mbeya. Nimewakuta watu wenye furaha hata kabla umeme haujawaka kwenye nyumba zao.

Nguzo za umeme kutoka Rujewa zimeshafika Nyeregete. Wanakijiji wana hamu wanaisubiri kwa hamu kubwa siku ile umeme utakawaka rasmi.

Kwao ina maana kubwa kuliko labda wengine tunavyofikiri. Umeme ni mkombozi wa kiuchumi. Wameshalijua hilo. Umeme utawaongezea maarifa mapya, hata kwa kuangalia televisheni tu.

Kuna mwanakijiji aliyeniambia: " Yaani, mie hata kama kulala na njaa, nitalala na njaa ili nipate fedha za kuingiza umeme! Nimechoka na vibatari na vitochi vya Mchina vye kuharibika mara kwa mara"

Na mwanakijiji mwingine anasema: " Hata kama kulipa laki mbili kuingiza umeme niko tayari!"

Na mwingine ananiambia: " .. Na Jumapili kwenye ibada , na yule ... anatwambia eti umeme wa nini wakati hamna maji ya bomba! Eti, anatwambia sisi hayo wakati yeye kwake ana umeme na huja hapa kanisani kututambia, kuwa mara ameona hiki na mara kile kwenye tv yake nyumbani!"

Na ninanachokiona mimi, na tafadhali usininukuu: Ni kuwa umeme huu wa vijijini utaisaidia CCM kubaki madarakani ifikapo Oktoba mwaka huu, lakini, wasipoweka mambo yao sawa na hususan kwenye usimamizi wa miradi ya maendeleo kwa wananchi, na hata kuwa na watendaji wasio waadilifu na zaidi mafisadi, basi, umeme huu wa vijijini, ndio utakaopelekea kwa kasi ya ajabu, kuiondoa CCM madarakani ifikapo 2020. Maana, umma wa vijijini, kupitia kwenye radio na runinga zao, nao utakuwa umemulikiwa maovu ya CCM kwa mwanga wa ' Umeme Vijijini'.

Maggid,
Iringa.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments