[wanabidii] KWANINI MNAAMINI KUWA YESU KAZALIWA BILA MARIA KUVUNJWA BIKIRA?

Thursday, September 11, 2014
BAADHI YETU KAMA WAAFRIKA TUNGALI TU WATUMWA PAMOJA NA UHURU TUNAOJIVUNIA.

Wengi wetu tumekuwa tukijivunia uislamu wetu au ukristo wetu sanjari na kudharau mambo ya mizimu yetu kama vile matambiko, ngoma zetu na hata lugha zetu.

Ni kweli iso shaka kuwa dini hizi za kiislamu na kikristo ni mila za watu uarabuni, uyaudi, na ulaya juhudi zao ndizo zilizopelekea mila hizi kusambaa duniani na kutufikia.

Sikatai wala kupinga kwa MWAFRIKA kuwa mkristo au muislamu, ninachopinga kwa mwafrika huyu kudharau uafrika wake na mila za mababu zetu kuziita ni ushetani na ya kwamba mwenye kufuata mila hizo ni mjinga na mpumbavu.

Mtu ukitambika au ukiomba kwa mujibu wa mila za kiafrika hili jambo lako fulani lifanikiwe basi wewe utaonekana kama mjinga au mchawi. Tena wanahoji iweje utegemee matambiko katika kushinda mtihani au usaili? Iweje uongeze bahati katika biashara yako kwa kutegemea matambiko?Tena watakuuliza, hivi hujui kuwa matambiko ni ushirikina?

Hawa wapumbavu washawahi kujiuliza maswahili haya pia? Hivi ni kwa kigezo gani hata miungu ya warabu na wayaudi ionekane bora kuliko miungu ya Afrika? Hivi kuna ushahidi gani wa kisayansi unaothibitisha kuwa hawa wanaoenda musikitini na makanisani kile wanachokiomba kinajibiwa? Hivi kuna tafauti gani kati ya yule aliyekesha kanisani ili ashinde usaili na yule aliyekwenda kukesha mzimuni ili ashinde usaili huohuo? Hivi kuna tafaut gani kati yule anayelala na biblia kwenye mchago wake na yule anayelala na hirizi? Hivi biblia au quran inamsaidiaje mtu dhidi ya mikosi au matatizo hata alale nayo au asome baadhi ya aya zake? Hivi imani alokuwa nayo mtu dhidi ya biblia au quran inatafaut gani na imani ya mtu mwingine dhidi ya hirizi?

Hivi iweje hasa aliyebeba kuku kwapani kupeleka mzimuni aonekane mjinga lakini aliyebeba fedha za sadaka kupeleka kanisani aonekane mwelevu? Hivi kwanini mtoa fungu la kumi au mzaliwa wa kwanza katika wanyama wake haonekane hana hila? Iweje hasa anayenawa maji ya baraka aoneka mmbora kuliko yule anatemewa maji mzimuni? Hivi iweje anayepewa leso au chumvi na mchungaj lwakatare aonekane mmbora lakini yule anayepewa mavumba aonekane mjinga? Hivi iweje zile kafara wanazitoa wayaudi, wakristo na waislamu kwa mungu wao zionekane sawa lakini zile za za mizimuni zionekane ujinga?

Hivi tunatumia vigezo gani katika kudharau dini na imani za kiafrika? Hivi tunatumia kugezo gani kuona imani za kiafrika urongo ikiwa hadi ninapoandika hii makala yangu KIAMA hakijatokea na wala hakuna dalili yake? Pia YESU HAJARUDI na wala hakuna dalili yoyote ya huyu Bwana kurudi? Tunatumia kigezo gani kusema Yesu anaponya ikiwa wachungaji, maaskofu, mapadri na waumini wao kila uchao wanakufa kwa ukimwi na malaria? Kwahiyo wanatudaganya kutangaza uponyaji ili hali wenyewe wanakufa?

Mtu anaamini mtoto kuzaliwa bila baba kisa kasoma kwenye kitabu chake au kaambiwa na mungu wake wa kiarabu au kiyaudi, lakini mtu huyo huyo haamini kuwa matambiko yetu yanaweza kumponya mtu na mikosi au kuleta mvua. Hivi ni jambo gani gumu kati ya mtoto kuzaliwa bila baba au kuleta mvua kwa matambiko? Hivi kwanini mnaamini kuwa Yesu kazaliwa bila baba lakini mnakuwa wazito kuamini matambiko ya kiafrika?

Waafrika tumekuwa wajinga kiasi cha kushindwa kuhoji au kujiuliza? Hivi binadamu kawa hayawani hata afanye mapenzi hadharani? Mna uhakika gani kama maria hakuanza kuvunjwa bikira kabla ya kumzaa yesu ikiwa kitendo cha ndoa hufanyika kwa faragha?

Sasa tuendelee kufuata na kuiga, yuleyule aliyetuletea ukristo kwa minajili ya kututawala ndio huyohuyo anatushurutisha kijanja turuhusu ushoga na ndoa zake. Tukijenga hoja kuwa ukristo unakataza ushoga watatujibu "huo ukristo tumewafundisha na ina maana mnaujua kuliko sisi wenyewe?" Mtajibu nini nyie waafrika wenzangu msojielewa?

Ndio maana Papa Francis leo hii anasema tuwaheshimu mashoga, kesho utasikia tuwafungishe ndoa. Kanisa Anglikana si kuruhusu tu lakini pia baadhi ya maaskofu wake wamejitangaza kushiriki ushoga. Sasa wenye dini yao wanaruhusu wewe ni nani hasa hata uzuie? Hizi ndio dini mnazojivuna nazo hata muuone uafrika ni ushenzi.

Njano5
0784845394

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments