Hizi ni baadhi ya kanuni za msingi za utendajiwa Jeshi la Polisi
Polisi hawapo kwa ajili ya kuwaadhibu watu, bali kwa ajili ya kuhakikisha kuwa watu wapo salama na sheria hazivunjwi.
Inapotokea kuwa polisi wanalazimika kudhibiti mkusanyiko wa watu, wanapaswa wahakikishe kuwa kila wakifanyacho wanatumia kiasi. Watalazimika kutumia nguvu kama suluhisho la mwisho baada ya hatua nyingine zote kushindikana. Hata hivyo, iwapo nguvu italazimika kutumika basi iwe ya kadiri na inayoendana na mazingira, na itumike kwa muda mfupi iwezekanavyo.
Matumizi ya Silaha za Moto dhidi ya Raia.
Kama ilivyosemwa hapo juu, polisi watatumia nguvu kubwa pale ambapo imelazimika tu, na ambapo njia nyingine zote za udhibiti zimejaribiwa na kushindikana.
Polisi anaweza kutumia bunduki katika mazingira yafuatayo:
Dhidi ya mtu anayetoroka, au
Dhidi ya mtu anayefanya jaribio la kutoroka toka kizuizini au
Dhidi ya mtu anayefanya jaribio la kutoroka asikamatwe
Dhidi ya mtu anayetumia nguvu kumwondoa mtu mwingine kutoka kizuizi halali
Dhidi ya mtu anayetumia nguvu kuzuia ukamatwaji halali wa mtu mwingine.
Dhidi ya kundi linaloharibu mali au kutishia usalama wa raia baada ya kuonya mara tatu
Lakini pale tu askari anapokuwa na sababu za msingi za kuamini kuwa hawezi kuzuia utoro huo kwa njia nyingine ana ametoa onyo kwa mtu huyo kuwa bunduki itatumika iwapo hatatii na mtu huyo hajali onyo lililotolewa. Pia endapo polisi watakuwa na sababu ya kuamini kuwa wao wenyewe wako hatarini kuumizwa vibaya.
Wanapolazimika kutumia bunduki dhidi ya kundi linalofanya uharibifu au kutishia usalama wa raia, risasi zinapaswa kulengwa chini na katika kundi linaloonekana ni tishio, lakini si kwa lengo la kusababisha mauaji bali kuwatawanya. Mara kundi linapoonyesha dalili la kutawanyika askari wanapaswa kusitisha upigaji risasi.
Polisi wanaolazimika kutumia risasi wanawajibika kutolea maelezo kila risasi waliyotumia kwa kuandika taarifa inayowekwa katika kumbukumbu.
Pale itakapothibitika kuwa polisi ametumia nguvu isiyohitajika atachukuliwa hatua za kinidhamu au kufunguliwa mashtaka kwa kosa la jinai
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments