Kutoka Lindi kuna taarifa ambayo imethibitishwa pia na kamanda Mpinga kuhusu ajali iliyotokea Mtwara ambayo imehusisha gari la Jeshi la Wananchi Tanzania(Jwtz)imeripotiwa asubuhi ya leo na shuhuda wa eneo hilo.
Msafara huo wa Wanajeshi ulikuwa ukitokea Mtwara kuelekea Nachingwea kwenye camp kubwa ya Jeshi na ajali hiyo imetokea maeneo ya Mnolela kijijini Lindi,kwa mujibu wa shuhuda ambaye ametoa taarifa hii kupitia kipindi cha Power Breakfast kutoka Clouds Fm amesema ajali hiyo imeua wanajeshi 3 na mwenye nyumba mmoja ambaye ni mwanamke alikua kalala ndani.
Madhara mengine yaliyotokana na ajali hii ni nyumba mbili kuharibika vibaya,majeruhi wa ajali hii wamepelekwa kwenye hospital ya Mkoa wa Mtwara.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments