[wanabidii] Taarifa ya mabadiliko ya muda wa saa za kazi katika ofisi za NHIF

Sunday, August 03, 2014
MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA (NHIF)

TAARIFA KWA UMMA


MABADILIKO YA MUDA WA SAA ZA KAZI KATIKA OFISI ZA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) unapenda kuwatangazia wadau wake na wananchi wote kwa ujumla kuwa umebadili muda wa saa za kazi kwa ofisi zake kote nchini. Mabadiliko haya yanatokana na ukweli kwamba wadau wa Mfuko wanawahi sana kufika ofisi za Mfuko kupata huduma. (Uzoefu wa Mfuko unaonyesha wadau hufika kabla ya saa 2 asubuhi kupata huduma).

Hivyo, kuanzia tarehe 1 Agosti 2014 ofisi za NHIF zitakuwa wazi kuanzia saa moja na nusu (1.30) asubuhi hadi saa kumi kamili (10:00) jioni kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa.

Huduma zote zinazotolewa na Mfuko zitaendela kutolewa kama kawaida muda huo na wote mnakaribishwa kuendelea kupata huduma za Mfuko kama kawaida.

NHIF: "Huduma bora za matiabau ni haki yako na ni dhamana yetu"

Kwa maelezo zaidi wasiliana na:

Kaimu Mkurugenzi Mkuu,

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya,

S.L.P.11360, Dar es Salaam; Simu: 022 2133969/964;

Barua pepe: info@nhif.or.tz; Tovuti: www.nhif.or.tz

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments