Wapendwa Wanabidii,
Naomba mnisaidie kupata ufafanuzi juu ya mambo kadhaa kuhusu mtangamano wa Afrika Mashariki kama ifuatavyo?
- Hivi kuna tofauti gani kati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Shirikisho la Afrika Mashariki?
- Katika mchakato wa mtangamano wa Afrika Mashariki (East African Integration) Watanzania katika makundi mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na kisiasa wamenufaikaje na mtangamano huo?
- Kuna haja ya nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashairiki kuingia kwenye ushirikiano wa kisiasa na kifedha? Mnadhani kunaweza kuwa na manufaa gani mahsusi kwa Watanzania?
- Kuna mambo yoyote ambayo yatatia hofu kwa Tanzania na Watanzania kuingia kwenda mbali zaidi kwenye huu ushirikiano?
Asanteni sana?
Sitta Peter
0 Comments