Rwanda ilikuwa eneo penye utawala wa kifalme tangu karne ya 16 BK kabla ya kufika kwa ukoloni. Mwanzo wake ni katika eneo la Ziwa la Muhazi. Watawala wenye cheo cha "mwami" kutoka kikundi cha wafugaji (Watutsi) walitanua himaya zao tangu miaka ya karne ya 16 BK hadi kufika eneo la leo hii. Wafugaji wa ng'ombe Watutsi walikalia nchi pamoja na wakulima wa Kihutu na wawindaji Watwaa.
UKOLONI WA KIJERUMANI
Ukoloni ulichelewa kufika Rwanda, mwaka 1890 Ujerumani na Uingereza walipatana ya kuwa Rwanda na Burundi ziwe ni sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Lakini ilikuwa mwaka 1908 tu ya kwamba Wajerumani walimtuma afisa wa kudumu aliyekaa Rwanda kama mwakilishi wa serikali ya Ujerumani. Mwaka 1916 Ubelgiji na Uingereza walivamia Rwanda katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Baadae ikawa chini ya Ubelgiji pamoja na Burundi kama "Rwanda-Urundi" katika hali ya eneo la kudhaminiwa kutokana na azimio la Shirikisho la Mataifa (UNO).
Utawala wa Wabelgiji ulikuwa wa moja kwa moja na mkali zaidi kuliko wa Wajerumani. Wabelgiji walijaribu kutoa faida ya kiuchumi wakilazimisha wenyeji kupanda mikahawa na kutekeleza kazi za serikali ya kikoloni. Katika utawala wao Wabelgiji walitumia zaidi Watutsi wakiwapa nafasi za elimu na kuwatumia katika shughuli za serikali. Wataalamu wengine huamini ya kwamba siasa hii ilisababisha kukua kwa chuki dhidi ya Watutsi kwa upande wa wakulima Wahutu iliyoleta kumwaga kwa damu baadaye.
Katika miaka ya 1950 ilionekana na kudhihirika ya kwamba ukoloni unaelekea mwisho wake. Uhusiano kati
UKOLONI WA KIJERUMANI
Ukoloni ulichelewa kufika Rwanda, mwaka 1890 Ujerumani na Uingereza walipatana ya kuwa Rwanda na Burundi ziwe ni sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Lakini ilikuwa mwaka 1908 tu ya kwamba Wajerumani walimtuma afisa wa kudumu aliyekaa Rwanda kama mwakilishi wa serikali ya Ujerumani. Mwaka 1916 Ubelgiji na Uingereza walivamia Rwanda katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Baadae ikawa chini ya Ubelgiji pamoja na Burundi kama "Rwanda-Urundi" katika hali ya eneo la kudhaminiwa kutokana na azimio la Shirikisho la Mataifa (UNO).
Utawala wa Wabelgiji ulikuwa wa moja kwa moja na mkali zaidi kuliko wa Wajerumani. Wabelgiji walijaribu kutoa faida ya kiuchumi wakilazimisha wenyeji kupanda mikahawa na kutekeleza kazi za serikali ya kikoloni. Katika utawala wao Wabelgiji walitumia zaidi Watutsi wakiwapa nafasi za elimu na kuwatumia katika shughuli za serikali. Wataalamu wengine huamini ya kwamba siasa hii ilisababisha kukua kwa chuki dhidi ya Watutsi kwa upande wa wakulima Wahutu iliyoleta kumwaga kwa damu baadaye.
Katika miaka ya 1950 ilionekana na kudhihirika ya kwamba ukoloni unaelekea mwisho wake. Uhusiano kati
ya Wahutu na Watutsi ukawa vigumu kwa sababu Wabelgiji walibadilisha siasa yao yakupendelea Watutsi wakidai haki zaidi kwa ajili ya Wahutu waliokuwa wengi. Ni hasa wamisionari wa katoliki Mapadre Weupe waliosimama upande wa Wahutu wakiona ndio wagandamizwa.
Mwami Mutara Rudahigwa aliyejiita pia Charles alijaribu kuleta upatanishi kati ya vikundi katika nchi. 1954 aligawa nchi ya kifalme kati ya Wahutu na Watutsi. Lakini alikuwa na wapinzani Watutsi waliomua mwaka 1959. Mtoto wake Mwami Kigeri V. alisimikwa kwenye kiti hicho. Hatua hii ilisababisha ghasia na vurugu nchini kwa sababu Wahutu walidai kuwa na neno katika mabadiliko ya serikali. Mwezi wa Novemba 1959 Mwami Kigeri V. alilazimishwa kuondoka nchini akikimbilia Uganda. Watutsi wenye siasa kali walijaribu kumwua kiongozi wa Mouvement Democratique Republicain (MDR) chama kikubwa cha Wahutu. Wahutu walijibu kwa kuwashambulia na kuua Watutsi. Wabelgiji walitumia wanajeshi wao kupoza hali hiyo nchini Rwanda. Katika uchaguzi wa kwanza wa halmashauri ya tarafa na miji kabla ya uhuru chama cha Parmehutu ndicho kilichopata kura nyingi. Viongozi wa Parmehutu walitangaza serikali mpya mwaka 1961. Uchaguzi wa Bunge ulileta kura ya 77% kwa ajili ya chama cha Parmehutu kilichomchagua kiongozi wake Grégoire Kayibanda kuwa Rais.
Tarehe 01.07.1962 Rwanda ilipata uhuru wake kamili. Wakati huo zaidi ya Watutsi 350,000 tayari walishakuwa wamekimbilia nchi za jirani. Mwaka uliofuata vikundi vya Watutsi kutoka nchi hizo za jirani walijaribu kufanya mapinduzi kwa kushambulia serikali mpya wakitokea uhamishoni. Kitendo hicho kilifuatiwa na uangamizaji wa kwanza wa Watutsi zaidi ya 100,000 waliouawa na Wahutu.
Hata katika miaka iliyofuata mauaji dhidi ya Watutsi iliendelea. Wanasiasa Wahutu walizoea kuita Watusi ndio "Wadudu". Kila kitu kilichokuwa si sawa kilielezwa ni kosa la Watutsi waliokuwa raia bila haki. Idadi kubwa ya Watutsi walikimbia Burundi, Uganda na Tanzania.
Mwaka 1973 Generali Habariyama alimpindua rais Kayibanda na kuanzisha serikali ya kijeshi akijaribu kupatanisha vikundi ndani ya taifa. Lakini hata mwaka uliofuata 1974 mauaji ya Watutsi yalitokea tena.
Mnamo 1990 ilikuwa wazi ya kwamba Rwanda ilikuwa na hali ngumu. Kwa upande moja nchi za mataifa zilisukuma serikali za Afrika kuruhusu kura huru za kisiasa.
Katika Rwanda ongezeko la wakazi lilileta msongamano mkubwa na uhaba wa ardhi ya kilimo na Ufugaji. Uchumi ulikuwa duni, Wakati huohuo wapinzani Wahutu walikusanyika nje ya nchi hiyo kudai demokrasia. Na katika makumi elfu ya watoto wa Watutsi waliokuwa nje ya nchi hiyo, sauti zikasikika zilizodai warudi tena kuijenga Rwanda.
Habyarimana alijaribu kutafuta suluhisho na ungamano wa kitaifa, akaanza kujadiliana na Watutsi wa nje lakini alikutana na upinzani kwa upande wa Wahutu wakali waliochukia uelewano na Watutsi.
Safari ya Kagame na RPF kurudu Rwanda kutoka Uganda.
Oktoba 1990 Watutsi waliokaa Uganda walianzisha chama cha RPF (Rwanda Patriotic Front) wakiwa na wafuasi wahutu wachache wakavamia Rwanda kwa silaha. Kiongozi wao alikuwa Paul Kagame aliyeondoka Rwanda akiwa mtoto wa miaka minne. Alikuwa amejiunga na jeshi la Yoweri Museveni na kupanda ngazi katika jeshi la Uganda hadi kuwa mkuu wa huduma ya usalama ya kijeshi ya Uganda. Walitaka kulazimisha serikali ibadilishe hali ya Watutsi kuwa raia bila haki. Lakini uvamizi huu ulisababisha kuongezeka kwa ukali wa Wahutu dhidi ya Watutsi ndani ya Rwanda na siasa kali kwa upande wa viongozi Wahutu. Kikundi cha kihutu cha Interahamwe kilipewa silaha kujibu mapigo dhidi ya uvamizi wa Kagame, Maelfu ya Watutsi Warwanda waliuawa. Vita kati ya wapinzani kutoka Uganda na jeshi la serikali iliendelea mpakani hadi pande zote mbili zilikutana hapa Arusha Tanzania na kupatana kukoma kwa vita 1992 chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika.
Sehemu ya viongozi Warwanda walijiandaa kutafuta utaratibu mpya lakini wengine walifanya mipango ya kumaliza swali la Watutsi kabisa wakipanga kuua Watutsi wote nchini.
Tarehe. 06.04.1994 rais Habariyama akirudi nchini kutoka safari ya Tanzania, Ndege yake ilipigwa kombora kabla ya kutua ikaanguka chini akafariki. Uwezekano ni mkubwa ya kwamba ni Wahutu wenye msimamo mkali ndio waliomua, lakini wengine walisema ni Jenerali Paul Kagame na RPF yake.
Tendo hili ilikuwa mwanzo wa mauaji ambayo hayakuwahi kutokea Afrika. Viongozi wa Interahamwe, wa jeshi la kitaifa na vikundi vikali vya Kihutu walitekeleza mipango ya kukusanya Watutsi kila mahali na kuwaua. Haiwezekani kuwa na idadi kamili lakini makadirio ya chini yanataja Watutsi 750.000 na Wahutu wasio wakali zaidi ya 100.000 waliuawa na Interahamwe na wanajeshi wa serikali ya Kihutu. Watu walikimbilia na kutafuta hifadhi makanisani lakini hata huko walichinjwa bila neema. Wahutu waliokataa kushiriki katika mauaji waliuawa pia.
RPF chini ya uongozi wa Paul Kagame iliamua kutumia nguvu zote kusimamisha machinjo haya. Kwa miezi miwili mauaji na vita yalienda sambamba hadi RPF iliposhinda Julai 1994 na kuchukua madaraka ya serikali.
Jeshi, Waparmehutu na serikali ya Kihutu walikimbilia Kongo wakiwalazimisha wakazi wengi kuongozana nao hali iliyosababisha kutokea kwa makambi ya wakimbizi makubwa sana katika Kongo ya mashariki yaliyokuwa na idadi ya Wahutu milioni mbili. Walio wengi wamerudi baada ya kuimarika kwa serikali mpya.
Tangu ushindi wa kijeshi mwaka 1994, RPF walianzisha serikali ya umoja wa kitaifa. Rais alikuwa Pasteur Bizimungu mwanasiasa Mhutu aliyeshikamana na RPF Kagame akiwa makamu wake. Baada ya kupinduliwa kwa Bizimungu mwaka 2000 Kagame akawa Rais. 2003 palitokea uchaguzi wa kwanza wa kirai ambapo chama cha RPF chimi ya Jenerali Paul Kagame kilishinda.
Jeshi la Rwanda limeendelea kuwa na vita ndani ya Kongo likipigana na mabaki ya Interahamwe waliokuwa wanashambulia Rwanda mara kwa mara kutoka Kongo.
Kutokana na mauaji hayo ya 1994, mahakama ya kimataifa iliyopo nchini Uholanzi imeendesha hukumu nyingi kwa wahusika wake, vilevile mahaka ya kimataifa ya Arusha nchini Tanzania nayo imeendesha huku stahiki kwa wahusika,
Ndani ya Rwanda mahakama za vijijini zinazoitwa "gachacha" vilevile zimejaribu kutoa hukuma juu ya waliohusija na mauaji ya mwaka 1994.
Mapatano ndani ya Rwanda yamezidi kushamiri, huku Paul Kagame akionsha kuijenga vema Rwanda kwa mkono wa chuma, Mathalani: D.Gasangwa wa EACU arisisitiza kwamba "Sometime in April(2004)" movie, ilikuwa "ETHNIC CLEASING", si HOLOCOSTI!, kama ilivyoandikwa na Wazungu wa Magazeti ya Ulaya. Watu karibu 600,000 waliuawa Rwanda, na hapo Mkoa wa Kivu, Congo.
Afrika ina ujuzi sasa; kama ujuzi wa Kiarabu, Kiswahili, Kilingala, Kiwolof, Kiamharic. Utengamano wa siasa mpya rasima utatupa na fasi ya kujenga inchi mpya kama EACU na Rwanda Kazembe.
Lakini huku mapambazuko mema yakitamalaki Rwanda, Kiongozi wa utawala wa nchi hiyo ndogo, anatajwa kuwa ni miongozi mwa viongozi makupe barani Afrika, ukupe wake sio waufisadi bali ukwasi wenye chembe za kiyunani
Lakini leo yale mabaki ya vikundi vile vya Interahamwe vilivyokimbilia uhamishoni kaskazini mwa Kongo mji wa Goma na Kivu si vikundi vya uasi dhidi ya Rwanda tena bali ni vitendea kazi muhimu dhidi ya upanuzi wa miliki mpya ya Watusi,
Wale watusi waliokimbilia Uganda enzi za Mwami Kigeri V, Inatajwa na kuaminika kuwa Jenerali Paul Kagame, Yoweri Mseveni na Watutsi waliokimbilia Goma baada ya kushika dola zao, walikuja na malengo mujarabu yanayotekelezwa kwa hatua na kwa vipindi virefu sana,
Mpango huo ulikuwa ni kusimika dola imara la Watutsi barani Afrika hasa nchini Kongo katika Goma-Kivu ya Kasiskani mpango siri walioupa jina la "Nchi mpya ya ahadi ya Watutsi". Ni mpango endelevu ulio na lengo la kuwakusanya Watutsi duniani kote na kuwaweka pamoja wakimiliki ardhi na rasilimali zake!
Hili linathibitika katika kile walicho "Mkataba wa kuigawa Kongo" ulisainiwa na Yoweri Mseveni, Paul Kagame na Laurent Kabila akiomba msaada wa kuingia madarakani kwa mtutu wa bunduki,
Naam baada ya Laurent Kabila kuingia madarakani kwamsaada wa Kagame na Mseveni kupitia ule mkataba, Kabila alikataa kuheshimu mkataba ule nakusema yale yalikuwa ni maneno ya porini tu hivyo hawezi kuiuza nchi kwa karatasi za mstuni!
Hapo sasa ndipo tunapoingia kwenye madhila ya Kongo tuliyoyaona tangu mauaji ya L. Kabila na tunayoyashuhudia hii leo chini ya J. Kabila, M23, Kagame na Mseveni.
---
Imeandikwa na:
YERICKO NYERERE
Mwami Mutara Rudahigwa aliyejiita pia Charles alijaribu kuleta upatanishi kati ya vikundi katika nchi. 1954 aligawa nchi ya kifalme kati ya Wahutu na Watutsi. Lakini alikuwa na wapinzani Watutsi waliomua mwaka 1959. Mtoto wake Mwami Kigeri V. alisimikwa kwenye kiti hicho. Hatua hii ilisababisha ghasia na vurugu nchini kwa sababu Wahutu walidai kuwa na neno katika mabadiliko ya serikali. Mwezi wa Novemba 1959 Mwami Kigeri V. alilazimishwa kuondoka nchini akikimbilia Uganda. Watutsi wenye siasa kali walijaribu kumwua kiongozi wa Mouvement Democratique Republicain (MDR) chama kikubwa cha Wahutu. Wahutu walijibu kwa kuwashambulia na kuua Watutsi. Wabelgiji walitumia wanajeshi wao kupoza hali hiyo nchini Rwanda. Katika uchaguzi wa kwanza wa halmashauri ya tarafa na miji kabla ya uhuru chama cha Parmehutu ndicho kilichopata kura nyingi. Viongozi wa Parmehutu walitangaza serikali mpya mwaka 1961. Uchaguzi wa Bunge ulileta kura ya 77% kwa ajili ya chama cha Parmehutu kilichomchagua kiongozi wake Grégoire Kayibanda kuwa Rais.
Tarehe 01.07.1962 Rwanda ilipata uhuru wake kamili. Wakati huo zaidi ya Watutsi 350,000 tayari walishakuwa wamekimbilia nchi za jirani. Mwaka uliofuata vikundi vya Watutsi kutoka nchi hizo za jirani walijaribu kufanya mapinduzi kwa kushambulia serikali mpya wakitokea uhamishoni. Kitendo hicho kilifuatiwa na uangamizaji wa kwanza wa Watutsi zaidi ya 100,000 waliouawa na Wahutu.
Hata katika miaka iliyofuata mauaji dhidi ya Watutsi iliendelea. Wanasiasa Wahutu walizoea kuita Watusi ndio "Wadudu". Kila kitu kilichokuwa si sawa kilielezwa ni kosa la Watutsi waliokuwa raia bila haki. Idadi kubwa ya Watutsi walikimbia Burundi, Uganda na Tanzania.
Mwaka 1973 Generali Habariyama alimpindua rais Kayibanda na kuanzisha serikali ya kijeshi akijaribu kupatanisha vikundi ndani ya taifa. Lakini hata mwaka uliofuata 1974 mauaji ya Watutsi yalitokea tena.
Mnamo 1990 ilikuwa wazi ya kwamba Rwanda ilikuwa na hali ngumu. Kwa upande moja nchi za mataifa zilisukuma serikali za Afrika kuruhusu kura huru za kisiasa.
Katika Rwanda ongezeko la wakazi lilileta msongamano mkubwa na uhaba wa ardhi ya kilimo na Ufugaji. Uchumi ulikuwa duni, Wakati huohuo wapinzani Wahutu walikusanyika nje ya nchi hiyo kudai demokrasia. Na katika makumi elfu ya watoto wa Watutsi waliokuwa nje ya nchi hiyo, sauti zikasikika zilizodai warudi tena kuijenga Rwanda.
Habyarimana alijaribu kutafuta suluhisho na ungamano wa kitaifa, akaanza kujadiliana na Watutsi wa nje lakini alikutana na upinzani kwa upande wa Wahutu wakali waliochukia uelewano na Watutsi.
Safari ya Kagame na RPF kurudu Rwanda kutoka Uganda.
Oktoba 1990 Watutsi waliokaa Uganda walianzisha chama cha RPF (Rwanda Patriotic Front) wakiwa na wafuasi wahutu wachache wakavamia Rwanda kwa silaha. Kiongozi wao alikuwa Paul Kagame aliyeondoka Rwanda akiwa mtoto wa miaka minne. Alikuwa amejiunga na jeshi la Yoweri Museveni na kupanda ngazi katika jeshi la Uganda hadi kuwa mkuu wa huduma ya usalama ya kijeshi ya Uganda. Walitaka kulazimisha serikali ibadilishe hali ya Watutsi kuwa raia bila haki. Lakini uvamizi huu ulisababisha kuongezeka kwa ukali wa Wahutu dhidi ya Watutsi ndani ya Rwanda na siasa kali kwa upande wa viongozi Wahutu. Kikundi cha kihutu cha Interahamwe kilipewa silaha kujibu mapigo dhidi ya uvamizi wa Kagame, Maelfu ya Watutsi Warwanda waliuawa. Vita kati ya wapinzani kutoka Uganda na jeshi la serikali iliendelea mpakani hadi pande zote mbili zilikutana hapa Arusha Tanzania na kupatana kukoma kwa vita 1992 chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika.
Sehemu ya viongozi Warwanda walijiandaa kutafuta utaratibu mpya lakini wengine walifanya mipango ya kumaliza swali la Watutsi kabisa wakipanga kuua Watutsi wote nchini.
Tarehe. 06.04.1994 rais Habariyama akirudi nchini kutoka safari ya Tanzania, Ndege yake ilipigwa kombora kabla ya kutua ikaanguka chini akafariki. Uwezekano ni mkubwa ya kwamba ni Wahutu wenye msimamo mkali ndio waliomua, lakini wengine walisema ni Jenerali Paul Kagame na RPF yake.
Tendo hili ilikuwa mwanzo wa mauaji ambayo hayakuwahi kutokea Afrika. Viongozi wa Interahamwe, wa jeshi la kitaifa na vikundi vikali vya Kihutu walitekeleza mipango ya kukusanya Watutsi kila mahali na kuwaua. Haiwezekani kuwa na idadi kamili lakini makadirio ya chini yanataja Watutsi 750.000 na Wahutu wasio wakali zaidi ya 100.000 waliuawa na Interahamwe na wanajeshi wa serikali ya Kihutu. Watu walikimbilia na kutafuta hifadhi makanisani lakini hata huko walichinjwa bila neema. Wahutu waliokataa kushiriki katika mauaji waliuawa pia.
RPF chini ya uongozi wa Paul Kagame iliamua kutumia nguvu zote kusimamisha machinjo haya. Kwa miezi miwili mauaji na vita yalienda sambamba hadi RPF iliposhinda Julai 1994 na kuchukua madaraka ya serikali.
Jeshi, Waparmehutu na serikali ya Kihutu walikimbilia Kongo wakiwalazimisha wakazi wengi kuongozana nao hali iliyosababisha kutokea kwa makambi ya wakimbizi makubwa sana katika Kongo ya mashariki yaliyokuwa na idadi ya Wahutu milioni mbili. Walio wengi wamerudi baada ya kuimarika kwa serikali mpya.
Tangu ushindi wa kijeshi mwaka 1994, RPF walianzisha serikali ya umoja wa kitaifa. Rais alikuwa Pasteur Bizimungu mwanasiasa Mhutu aliyeshikamana na RPF Kagame akiwa makamu wake. Baada ya kupinduliwa kwa Bizimungu mwaka 2000 Kagame akawa Rais. 2003 palitokea uchaguzi wa kwanza wa kirai ambapo chama cha RPF chimi ya Jenerali Paul Kagame kilishinda.
Jeshi la Rwanda limeendelea kuwa na vita ndani ya Kongo likipigana na mabaki ya Interahamwe waliokuwa wanashambulia Rwanda mara kwa mara kutoka Kongo.
Kutokana na mauaji hayo ya 1994, mahakama ya kimataifa iliyopo nchini Uholanzi imeendesha hukumu nyingi kwa wahusika wake, vilevile mahaka ya kimataifa ya Arusha nchini Tanzania nayo imeendesha huku stahiki kwa wahusika,
Ndani ya Rwanda mahakama za vijijini zinazoitwa "gachacha" vilevile zimejaribu kutoa hukuma juu ya waliohusija na mauaji ya mwaka 1994.
Mapatano ndani ya Rwanda yamezidi kushamiri, huku Paul Kagame akionsha kuijenga vema Rwanda kwa mkono wa chuma, Mathalani: D.Gasangwa wa EACU arisisitiza kwamba "Sometime in April(2004)" movie, ilikuwa "ETHNIC CLEASING", si HOLOCOSTI!, kama ilivyoandikwa na Wazungu wa Magazeti ya Ulaya. Watu karibu 600,000 waliuawa Rwanda, na hapo Mkoa wa Kivu, Congo.
Afrika ina ujuzi sasa; kama ujuzi wa Kiarabu, Kiswahili, Kilingala, Kiwolof, Kiamharic. Utengamano wa siasa mpya rasima utatupa na fasi ya kujenga inchi mpya kama EACU na Rwanda Kazembe.
Lakini huku mapambazuko mema yakitamalaki Rwanda, Kiongozi wa utawala wa nchi hiyo ndogo, anatajwa kuwa ni miongozi mwa viongozi makupe barani Afrika, ukupe wake sio waufisadi bali ukwasi wenye chembe za kiyunani
Lakini leo yale mabaki ya vikundi vile vya Interahamwe vilivyokimbilia uhamishoni kaskazini mwa Kongo mji wa Goma na Kivu si vikundi vya uasi dhidi ya Rwanda tena bali ni vitendea kazi muhimu dhidi ya upanuzi wa miliki mpya ya Watusi,
Wale watusi waliokimbilia Uganda enzi za Mwami Kigeri V, Inatajwa na kuaminika kuwa Jenerali Paul Kagame, Yoweri Mseveni na Watutsi waliokimbilia Goma baada ya kushika dola zao, walikuja na malengo mujarabu yanayotekelezwa kwa hatua na kwa vipindi virefu sana,
Mpango huo ulikuwa ni kusimika dola imara la Watutsi barani Afrika hasa nchini Kongo katika Goma-Kivu ya Kasiskani mpango siri walioupa jina la "Nchi mpya ya ahadi ya Watutsi". Ni mpango endelevu ulio na lengo la kuwakusanya Watutsi duniani kote na kuwaweka pamoja wakimiliki ardhi na rasilimali zake!
Hili linathibitika katika kile walicho "Mkataba wa kuigawa Kongo" ulisainiwa na Yoweri Mseveni, Paul Kagame na Laurent Kabila akiomba msaada wa kuingia madarakani kwa mtutu wa bunduki,
Naam baada ya Laurent Kabila kuingia madarakani kwamsaada wa Kagame na Mseveni kupitia ule mkataba, Kabila alikataa kuheshimu mkataba ule nakusema yale yalikuwa ni maneno ya porini tu hivyo hawezi kuiuza nchi kwa karatasi za mstuni!
Hapo sasa ndipo tunapoingia kwenye madhila ya Kongo tuliyoyaona tangu mauaji ya L. Kabila na tunayoyashuhudia hii leo chini ya J. Kabila, M23, Kagame na Mseveni.
---
Imeandikwa na:
YERICKO NYERERE
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 Comments