WAKALA WA MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI
MATUMIZI YA TEKNOLOJIA YA VINASABA VYA BINADAMU, TANZANIA
JULY, 2013
1.0 UTANGULIZI
Tekinolojia ya vinasaba vya binadamu inafanya kazi kwa kusimamiwa na sheria namba 8, sura ya 73, ya mwaka 2009. Sheria hiyo inaitwa The Human DNA Regulation Act, [Cap 73, 2009] ambayo inasimamia na kudhibiti matumizi ya tekinolojia ya vinasaba vya binadamu.
Mkemia Mkuu wa Serikali ndiye msimamizi wa utekelezaji wa sheria hii.
Taarifa fupi ya umuhimu wa tekinolojia ya vinasaba vya binadamu inavyosaidia katika matukio mbalimbali nchini Tanzania.
2.0 UCHUNGUZI WA VINASABA
Uchunguzi unaohusisha tekinolojia ya vinasaba, unahusisha vielelezo vinavyotokana au kupatikana katika mashauri au matukio yafuatayo:
a. Mauaji
b. Majanga
c. Ubakaji
d. Wizi /Wizi wa kutumia silaha.
e. Uhamiaji
f. Uhalali wa mzazi kwa mtoto
g. Utambuzi wa binadamu
h. Utambuzi wa Jinsi Tawala
3.0 MIFANO HALISI YA MATUMIZI YA TEKINOLOJIA YA VINASABA VYA BINADAMU
Baadhi ya matukio au mashauri yaliyohusisha matumizi ya Tekinolojia ya vinasaba vya binadamu yamechanganuliwa kama ifuatavyo:
MATUMIZI YA TEKNOLOJIA YA VINASABA VYA BINADAMU, TANZANIA
JULY, 2013
1.0 UTANGULIZI
Tekinolojia ya vinasaba vya binadamu inafanya kazi kwa kusimamiwa na sheria namba 8, sura ya 73, ya mwaka 2009. Sheria hiyo inaitwa The Human DNA Regulation Act, [Cap 73, 2009] ambayo inasimamia na kudhibiti matumizi ya tekinolojia ya vinasaba vya binadamu.
Mkemia Mkuu wa Serikali ndiye msimamizi wa utekelezaji wa sheria hii.
Taarifa fupi ya umuhimu wa tekinolojia ya vinasaba vya binadamu inavyosaidia katika matukio mbalimbali nchini Tanzania.
2.0 UCHUNGUZI WA VINASABA
Uchunguzi unaohusisha tekinolojia ya vinasaba, unahusisha vielelezo vinavyotokana au kupatikana katika mashauri au matukio yafuatayo:
a. Mauaji
b. Majanga
c. Ubakaji
d. Wizi /Wizi wa kutumia silaha.
e. Uhamiaji
f. Uhalali wa mzazi kwa mtoto
g. Utambuzi wa binadamu
h. Utambuzi wa Jinsi Tawala
3.0 MIFANO HALISI YA MATUMIZI YA TEKINOLOJIA YA VINASABA VYA BINADAMU
Baadhi ya matukio au mashauri yaliyohusisha matumizi ya Tekinolojia ya vinasaba vya binadamu yamechanganuliwa kama ifuatavyo:
s/n | Aina ya tukio | TUKIO | Matumizi ya Tekinolojia ya vinasaba vya binadmu | Maoni/hoja |
3.1 | Mauaji ya Albino na Vikongwe | · SHINYANGA-3(2009) · KAGERA-3(2009) · SUMBAWANGA-2(2013) | Kesi mbili(2) tayari zilishatolewa hukumu kutegemea na matokeo ya uchunguzi wa DNA | |
| | | | |
3.2 | Majanga | · Milipuko-Mbagala(2010) DAR · Moto: Shule ya Idodi-IRINGA · Kuanguka kwa Jengo- Mtaa wa Kisutu.(2013). · Ajali ya Ndege Comoro.(2010)-Mafia/Dar | Askari 6 walitambuliwa na mabaki ya marehemu kuchukuliwa na ndugu wa Marehemu kwa ajili ya kuzikwa. Mabaki ya Marehemu, wanafunzi 12 walitambuliwa na makaburi kutambuliwa. Mabaki ya sehemu ya miili ya marehemu 23 yaliweza kutambuliwa Mabaki ya miili ya marehemu 25 iliweza kutambuliwa na ndugu kuchukua kwa ajili ya kuzika | |
| | | | |
3.3 | Ubakaji/Mimba za utotoni. | Mkoa wa MBEYA –(2013) | Uchunguzi umesaidia upelelezi na Mahakama Katika kesi za kuwapa mimba mwanafunzi wa shule/wasichana chini ya umri 18. | |
3.4 | Uhamiaji | · Mbeya · Ngara-Kagera: Mwanachi kutoka nchi nya nje kudai kuwa na uhusiano na na ndugu ntanzania | Tekinolojia ya vinasaba ilitumika na kudhihirisha kuwa hawana uhusiano na wananchi waliowataja nchini Tanzania | |
| | | | |
3.5 | Wizi/wizi wa kutumia silaha | · Wizi wa benki NMB(2006) · Wizi wa benki ya West Bureau De Change | Uchunguzi umesaidia upelelezi na Mahakama katika kubaini wa husika | |
| | | | |
3.6 | Human trafficking (biashara haramu ya binadamu) | · Miili ya binadamu iliyopatikana: Morogoro · Dodoma · Kibaha | Utambuzi wa binadamu kwa miili iliyopatokana | |
| | | | |
3.7 | Uhalali wa mzazi kwa mtoto | Katika kipindi cha Mwaka 2010-2012: | 51.68%-Kuhusisha(watoto ni wao) 48.32%-Kutohusisha(watoto sio wao) | |
| | | | |
3.8 | Utambuzi wa Jinsi tawala | Katika kipindi cha Mwaka 2010-2012 | 2.49%-Utambuzi wa jinsi tawala | |
4.0 MATARAJIO YA BAADAE
Mkemia Mkuu wa Serikali kupitia wizara mama ya Afya na Ustawi wa Jamii inamatarajio yafuatayo:
i. Kuhusisha Nyanja za tafiti
ii. Kuwepo kwa database ya vinasaba vya binadamu
iii. Usajili na ukaguzi wa taasisi zinahusisha matumizi ya tekinolojia ya vinasaba vya binadamu
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 Comments