[Mabadiliko] Historia Ya Kombe La Dunia ( IV); Italia 1934, Mcheza Kwao Hutuzwa....

Wednesday, June 26, 2013

Na Maggid Mjengwa,

Jana tulianza kwa kuzingalia fainali za pili za Kombe la Dunia
zilizofanyika nchini Italia maka 1934. Tulisema,  kama fainali za kwanza za
mwaka 1930 kule Uruguay zilionekana ni za majaribio, basi, fainali za pili
za  Kombe la Dunia  zilikuwa ni fainali za "kweli kweli".

Naam, enyi wapenzi wa soka, tutakumbushana , kuwa nchi ya Misri
ilikuwa ni taifa la kwanza barani Afrika kututoa mchanga wa macho kwa
kushiriki fainali hizi za Italia.

Katika fainali hizo, ingawa Misri  ilitolewa raundi ya kwanza ya mechi za mtoano,  ilifanikiwa kupachika  nyavuni magoli mawili ya kihistoria yaliyofungua mlango kwa bara hili kwenye kandanda ya dunia. Ilikuwa ni katika mechi kati ya Misri na Hungary ambapo  Misri ilibugizwa magoli 4-2 mjini Naples.

Magoli hayo mawili ya Misri yalifungwa na mshambuliaji aliyeitwa  Fawzi. Misri hawakuwa peke yao katika kutolewa kwenye raundi hiyo ya kwanza.  Walisindikizwa na nchi kama Brazil na Argentina, nchi zilizokuwa na majina makubwa katika kandanda hata wakati huo.
 

Ajabu katika fainali hizo za Italia ni kwa bingwa mtetezi, Uruguay
kususia kushiriki na kutetea taji lake..... Soma zaidi...http://www.mjengwablog.com/michezo/item/3534-hstoria-ya-kombe-la-dunia-iv-italia-1934-mcheza-kwao-hutuzwa.html#.UcsdNpyNCAg

--
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la 'Mabadiliko'.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda; mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com
Utapokea Email ya kudhibitisha kujiondoa kwako.
 
TEMBELEA Facebook yetu:
http://www.facebook.com/MabadilikoForums?ref=hl
 
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
 
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mabadiliko Forums" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

Share this :

Related Posts

0 Comments