Taarifa fupi...........
Leo mtangazaji wa BBC London, Suzana Machibya, amefanya mahojiano na wahusika wafuatao:
1. Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini akiwa Tanzania;
2. Padri Pauline Mundo wa Nairobi, Kenya;
3. Mwananchi wa kawaida, Mobhare Matinyi, akiwa Washington DC.
Mjadala ulihusu uteuzi wa kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis I. Kijumla majadiliano hayo ya karibu nusu saa yalihusu matarajio ya walimwengu kama miye na waumini na hata viongozi wa kanisa kwa kiongozi huyu mpya.
Ukipenda kusikiliza, vizia kesho saa 12 asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki, au baadaye kwenye Intaneti unaweza kufungua hapa: http://www.bbc.co.uk/swahili/kwa_kina/programme_archive_01.shtml na kisha kubonyeza kwenye "vipindi vya redio" au siku ikipita, nenda hapo hapo, kisha bonyeza kwenye "tazama ratiba nzima ya redio" na utapelekwa hapa, halafu bofya kwenye siku ya Jumamosi asubuhi, nadhani "amka na BBC"...... http://www.bbc.co.uk/swahili/kwa_kina/programme_archive_01.shtml.
Mjadala ulikuwa mzuri kwa mujibu wa mtangazaji mwenyewe wa BBC na nakumbuka moja ya matarajio yangu niliyoyataja ni kwamba Papa Francis I hatakubaliana na watu wanaotaka eti ndoa za jinsia moja zihalalishwe. Kulikuwa mijadala mingi, haya ni madodoso tu.
Asante,
Matinyi.
Leo mtangazaji wa BBC London, Suzana Machibya, amefanya mahojiano na wahusika wafuatao:
1. Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini akiwa Tanzania;
2. Padri Pauline Mundo wa Nairobi, Kenya;
3. Mwananchi wa kawaida, Mobhare Matinyi, akiwa Washington DC.
Mjadala ulihusu uteuzi wa kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis I. Kijumla majadiliano hayo ya karibu nusu saa yalihusu matarajio ya walimwengu kama miye na waumini na hata viongozi wa kanisa kwa kiongozi huyu mpya.
Ukipenda kusikiliza, vizia kesho saa 12 asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki, au baadaye kwenye Intaneti unaweza kufungua hapa: http://www.bbc.co.uk/swahili/kwa_kina/programme_archive_01.shtml na kisha kubonyeza kwenye "vipindi vya redio" au siku ikipita, nenda hapo hapo, kisha bonyeza kwenye "tazama ratiba nzima ya redio" na utapelekwa hapa, halafu bofya kwenye siku ya Jumamosi asubuhi, nadhani "amka na BBC"...... http://www.bbc.co.uk/swahili/kwa_kina/programme_archive_01.shtml.
Mjadala ulikuwa mzuri kwa mujibu wa mtangazaji mwenyewe wa BBC na nakumbuka moja ya matarajio yangu niliyoyataja ni kwamba Papa Francis I hatakubaliana na watu wanaotaka eti ndoa za jinsia moja zihalalishwe. Kulikuwa mijadala mingi, haya ni madodoso tu.
Asante,
Matinyi.
0 Comments