[wanabidii] TAMKO LA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA WA MBEYA KUHUSU UCHOCHEZI WA KIDINI

Friday, February 22, 2013
TAMKO LA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA WA MBEYA KUHUSU UCHOCHEZI WA
KIDINI


Kwanza kabisa tungependa kutoa pongezi kwa Viongozi na Waumini wa Dini
na Madhehebu mbalimbali hapo Mkoa Mbeya kuendeleza utamaduni wetu wa
kuishi na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii. Bila
kuweka hisia za udini. Tunawashukuru kwa kuendelea kuvumiliana. Pamoja
na kuendelea katika hali hii, kumejitokeza viashiria mbalimbali vyenye
kuonyesha dalili za kumomonyoka kwa maadili, katika Mkoa wetu.

2. Kumejitokeza baadhi ya viongozi wa dini ambao wamekuwa Wakuzitumia
nyumba zetu takatifu za Ibada kuhubiri mambo ambayohayahusiani kabisa
na mambo yanayohusu Mwenyezi Mungu na mafundisho yake, kwa kuhubiri
mambo ya siasa za chuki kwa dhamira ya kupandikiza chukidhidi ya
Serikali au dini na madhehebumengine. Baadhi yao wamediriki kuyasema
hayo hadharani kwenye miadhara yao au mikusanyiko ya waumini wao.

Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya inaona hali hii haina afya
njema kwa mustakabali wa amani na utulivu wa Mkoa wetu na Nchi kwa
ujumla.

3. Pamoja na mahubiri hayo pia kumekuwepo nyaraka mbalimbali za
kimaandishi za sauti katika kanda, CD zenye kuhubiri chuki, uchochezi
dhidi ya dini au dhehebu lingine. Kumekuwepo na video katika kanda, CD
au DVD zenye kuhubiri chuki, uchochezi, dharau na kebehi dhidi ya dini
nyingine au Serikali na baadhi ya kanda hizo zimediriki kuhamasisha
waumini wake vurugu na hata kuua jambo ambalo Kamti ya Ulinzi na
Usalama Mkoa wa Mbeya inaamini hakuna dini ya aina yoyote
dunianiinayohimiza waumini wote kutumia kwa jambo lolote lile.

4. Baada ya kutafakari, Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya
imeamua yafuatayo:- inapiga marufuku:

(i) Kuuza, kusambaza au kuonyesha, Kanda za sauti CD za sauti, Kanda
za Video, CD, DVD, nyaraka na maandiko yoyte yenye uchochezi wa aina
yoyote ile au kukashifu dini yeyote katika Mkoa wa Mbeya.

(ii) Chombo chochote cha Habari kilichopo Mkoani Mbeya kiepuke
kuandika makala, kunakili au kurusha hewani hotuba, mahubiri au
kuonyesha video zenye kuchochea, kudharau, kuhubiri au kukashifu dini
yoyote ile

5. Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa inawaasa viongozi wa dini
Mbalimbali kutohubiri siasa kwenye majumba ya Ibada kwani kwa kufanya
hivyo watakuwa wanakiuka sheria za nchi. Mtawagawa waumini wenu kwa
sababu waumini wanaelewa hayo si maagizo ya Mungu, na hayamo kwenye
vitabu vitakatifu.

6. Waandishi wa Habari epukeni kushabikia matamko ya Viongozi wa Dini
au Siasa yenye kulenga kuleta mgawanyiko katika taifa hili kwa Misingi
ya kidini au kisiasa kwa kisingizio cha Uhuru wa Habari, kumbukeni
Amani Umoja na Mshikamano wa Mkoa na Taifa utategemea mchango wenu
katika kushabikia au kukemea kauli hizo bila kujali zimetolewa na
kiongozi gain.

Mwisho, Serikali itamchukulia hatua za kisheria mtu yeyote
atakayekwenda kinyume na haya, bila kujali itikadi yake, dini yake au
wadhifa wake. Wananchi wanaaswa kuzikabidhi nyaraka, kanda CD na DVD
kwa ofisi za Serikali ngazi ya Vijiji, kata Wilaya na Mkoa au kituo
chochote cha Polisi. Endapo watakabidhi kwa hiyari hawatachukuliwa
hatua.

Imetolewa na:

MWENYEKITI
KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA-MBEYA

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

Share this :

Previous
Next Post »
0 Comments