Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa ustahamilivu na uvumilivu wa Serikali umefikia kikomo kwa wale wote wanaofanya vitendo vya fujo na vurugu na itamshughulikia ipasavyo mtu yo yote atakaevunja sheria. Dk. Shein aliyasema hayo leo katika hotuba yake aliyoitoa kwenye Baraza la Idd el Hajj.Lililofanyika huko katika hoteli ya Bwawani mjini Zanzibar.Katika hotuba yake hiyo Dk. Shein alisema kuwa ustahamilivu na utulivu sio udhaifu ni heshima kubwa ya kutii amri ya Mwenyezi Mungu na kusisitiza kuwa hatua ya serikali kuvumilia vitendo hivyo vya uvunjifu wa amani sasa basi. "enough is enough", alisisitiza Dk. Shein.
Related Posts
- [wanabidii] Speaker's name
- [wanabidii] News Digest: Indian carmakers worry more about sales than safety
- [wanabidii] Police disinter Arabs from graves & arrests them, Jordan sends condolences to terrorists, Banning Abbas - Nov. 23, 2014
- [wanabidii] Fwd: Mapiku
- [Mabadiliko] Religious war???
- [Mabadiliko] Mdahalo 25.11.2014 Mlmani City.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Comments