[wanabidii] SEIF SHARRIF HAMAD APASUWA BOMU!!!

Monday, September 24, 2012
Dear All,
Makamo wa Rais wa Zanzibar ambae pia ni Katibu Mkuu wa CUF apasuwa bomu kwa CCM na kwa Watanganyika pale alipoweka
msimamo wake na wa CUF wazi kabisa kwa kutamka jana mkutanoni Bububu kuwa..."wakati umefika kwa Wazanzibari kuendesha nchi yao wenyewe 
ikiwa na mamlaka ya ndani na nje na mimi ni miongoni mwa Wazanzibari wanaounga mkono hatua hiyo".
"Wazanzibari wanataka kuendesha nchi yao yenye mamlaka kamili…mimi binafsi ni muumini wa Muungano wa mkataba,"
"Muungano wa mkataba utaturudishia haki zetu Wazanzibari na sasa hivi tuna Serikali, lakini leo Serikali yetu kila kitu 
lazima tukapige magoti Tanganyika," alisema na kufafanua zaidi kuwa:
"Tunataka Benki Kuu yetu ya Zanzibar na Tanganyika watakuwa na yao…halafu tukishapata Muungano wa mkataba Zanzibar itakuwa huru,....." 
"Inshallah kwa uwezo wa Mwenyenzi Mungu, Zanzibar itarudi katika mamlaka kamili…, Wazanzibari wanachokitaka ni kuungwa mkono na mataifa makubwa,"

Share this :

Related Posts

0 Comments