[wanabidii] maandamano

Sunday, February 07, 2016
Ulimwenguni watu wanaandamana wakiwa na sababu zinazoeleweka na ndio maana hupewa vibali vya kufanya hivyo na ofisi zinazohusika. Vibali hivyo havielezi nani anapaswa kushiriki au hapaswi kushiririki. Swala la mshiriki huwa mikononi ya walio tayarisha maandamano hayo. Iwapo vijana hao wanataka maandamano yawe tu ya wanaofanya kazi yeyote ile, basi ni wao katika matangazo yao ya kushiriki ndio wanapaswa kusema, vinginevyo na hivyo ni uonevu kutoa hoja ya wasiofanya kazi wasishiriki. Tukumbuke kodi zinazolipwa na raia zinatumika kwa shughuli mbali mbali na siyo tu ya TRANSMISSION za mijadala ya bungeni
Kisheria wananchi wanatakiwa kuelewa chochote kinachofanyika nchini kwao kupitia vyombo vya habari, mojawapo ikiwa TV. Sio kila mtu ana uwezo wa kununua magazeti kila siku na hatuna centres ambazo mtu unaweza kwenda ukasoma magazeti bure. Wabunge ni kiungo kati ya raia na serikali, ndio maana watu wanataka kuona live hao watu waliowachaguwa wanasema nini na maadili yanayofikiwa ni yapi na hivyo kuwapa motisha hata vijana katika shughuli zao za kila siku. Hakuna sababu ya kuficha mazuri au mabaya yanayotokea. Ufumbuzi unaweza kuwa rahisi wakati watu wanapokuwa wanaelewa wanachotakiwa kufanya kwa kupewa ukweli wa hali halisi.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments