Kumbe kinara wa kashfa ya Richmond alikuwa bosi wake. Lo! Sasa inaingia akilini ni kwa nini TOR za Mwakyembe hakikumuweka Lowassa kama sample ya kuhojiwa kashfa ya Richmond ilipotokea. Lakini kwa unyenyekevu Lowassa alijiuzulu kuinusuru serikali nzima isianguke. Mungu mwema miaka minane baadaye ukweli kamili wa Richmond unajulikana. Kama ulichokisema ni kweli Lowassa, Mungu atakupigania kwa sababu ni wewe na Mzee Mwinyi peke yenu mna rekodi ya kujiuzulu kuonyesha uwajibikaji kutokana na nafasi zenu na siyo kosa mlilolitenda ninyi wenyewe. Viongozi wengine mpaka umma upige kelele sana ndipo wajibaraguze kujiuzulu mfano kashfa ya escrow 2014. Sasa ninaelewa ni kwa nini baadhi ya watu wana hofu baada ya LOwassa kukubaliwa na UKAWA kuwa mgombea Urais.
Namshukuru sana aliyetuwekea hii you-tube huku jukwaani maana baadhi yetu ambao hatuko site tungeweza kuendelea kufanya uchambuzi wetu kwa kutumia habari nusu nusu tulizopewa miaka iliyopita kuhusu kashfa ya Richmond.
Ananilea Nkya
E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com
--
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la 'Mabadiliko'.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mabadiliko Forum" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
To post to this group, send email to mabadilikotanzania@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania.
To view this discussion on the web visit https://groups.google.com/d/msgid/mabadilikotanzania/1438213382.81730.YahooMailBasic%40web121001.mail.ne1.yahoo.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 Comments