[wanabidii] SERIKALI YAIFUNGIA FILAMU YA FIFTY SHADES OF GREY

Monday, February 16, 2015

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO

Simu: 2110585Jengo la PSPF Golden Jubilee Tower
Nukushi: 2113814 S.L.P 8031
Barua pepe: km@habari.go.tz7 Mtaa wa Ohio,
Tovuti: www.habari.go.tz11481 DAR ES SALAAM

TAARIFA KWA UMMA

Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza Tanzania inawaagiza Wamiliki wote wa kumbi za filamu Tanzania Bara kutofanya maonesho ya hadhara ya filamu yenye jina la FIFTY SHADES OF GREY inayoongozwa na Sam Taylor Johnson na kutengenezwa na Michael De Luka, Dana Brunetti na E.L. James.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza Tanzania kukagua filamu hiyo yenye urefu wa saa 2:05 na kugundua kwamba haizingatii sheria na kanuni zinazosimamia tasnia ya filamu nchini. Maamuzi haya yamefanywa kulingana na ukiukwaji wa Sheria ya Filamu na Michezo ya Kuigiza Na. 4 ya mwaka 1976 kifungu cha 15 (i) na kifungu 18(i na ii) ambayo ufafanuzi wa utekelezaji wake uko katika Kanununi za Sheria hiyo Kifungu cha 24 vifungu vidogo vya a,b,d,e,n na t.

Filamu ya FIFTY SHADES OF GREY hairuhusiwi kuonyeshwa popote Tanzania. Aidha, Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza Tanzania inawakumbusha kwa mujibu wa Sheria tajwa hapo juu Wamiliki wote wa kumbi za sinema na maeneo yote ya kuonyeshea filamu kuwasilisha filamu katika Bodi hiyo ili zikaguliwe na kupangiwa daraja kabla hazijaanza kuonyeshwa na kutofanya hivyo ni ukiukwaji wa sheria.

Pia uzinduzi wowote wa filamu unaofanywa katika kumbi za sinema na maeneo yoyote ya kuonyeshea filamu ni lazima uwe na kibari kutoka Bodi ya Ukaguzi wa Filamu na Michezo ya Kuigiza.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments