[wanabidii] DK.BILAL KUWEKA JIWE LA MSINGI CHUO KIKUU CHA BAGAMOYO KESHO

Friday, January 16, 2015
DK.BILAL KUWEKA JIWE LA MSINGI CHUO KIKUU CHA BAGAMOYO KESHO
* RAIS MKAPA ,MAASKOFU KUHUDHURIA

Na Happiness Katabazi (UB)
MAKAMU wa Rais ,Dk.Mohammed Gharib Bilal Kesho anatarajiwa Kuwa mgeni rasmi katika sherehe za uwekwaji wa jiwe la Msingi la Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB), zitakazofanyika katika Kijiji cha Kiromo,Bagamoyo Mkoani Pwani.

Akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake Mikocheni Dar es Salaam jana, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho anayeshughulikia Fedha na Utawala, Dk.Elifuraha Mtalo alisema sherehe hizo zitafanyika Katika Kijiji cha Kiromo na kwamba uwekwaji wa jiwe hilo ni ufunguzi rasmi wa ujenzi wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo Katika Kijiji hicho ambao unatarajiwa kuanza Mwaka huu.

Dk.Mtalo alisema Dk.Bilal ndiye atakuwa mgeni rasmi pia na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa naye anatarajiwa kuwa miongoni mwa wageni walioalikwa katika sherehe hiyo ya kihistoria katika Wilaya ya Bagamoyo kwasababu Somo la Historia linatufundisha kuwa mji wa Bagamoyo watumwa walikuwa wakiishi.

" UB tunaifahamu historia ya Mji wa Bagamoyo ndiyo maana tukaamua kuanzisha Chuo Kikuu ambacho tumekipa jina la University of Bagamoyo.Kupitia Mji wa Bagamoyo tulikuwa watumwa, hivyo kupitia UB ambayo inajenga makazi yake ya kudumu katika mji huo, binadamu wote watakuwa huru kwasababu tutapata elimu" alisema Dk.Mtalo.

Alisema UB ambayo ilianzishwa rasmi mwaka 2011 ambayo ina makazi yake yake ya muda ,Mikocheni B, Dar es Salaam na kwamba ujenzi wa Makazi ya kudumu ya UB kijijini Kilomo , utasaidia kukuza shughuli za uchumi, wananchi wa eneo hilo kupata huduma ya elimu ya ngazi ya Chuo Kikuu kwa ukaribu na ajira.

Aidha aliwaomba wananchi Wilaya Bagamoyo na Mkoa wa Pwani kwa ujumla kujitokeza kwa Wingi Katika sherehe hiyo.

Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Blogg: www.katabazihappy.blogspot.com
Januari 16 Mwaka 2015.


Sent from my iPad

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments