[wanabidii] Serikali yapokea mabehewa 22 ya abiria na 50 ya mizigo

Monday, December 08, 2014


Serikali imepokea mabehewa 50 ya mizigo na mabehewa 22 ya kisasa ya abiria ikiwa ni sehemu ya mabehewa 274 yanayotawarajiwa kuwasili nchini ili kuboresha huduma za usafiri wa mizigo na abiria.

Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe amesema kuingia kwa mabehewa hayo ni ishara ya jitihada za serikali katika kuimarisha huduma ya usafiri wa reli ambapo amesema serikali imetumia zaidi ya bilioni 200 katika kuboresha sekta ya reli nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la reli nchini, Kipalo Kisamfu amesema mabehewa hayo ya abiria ni kwa ajili ya safari katika mikoa ya Mwanza na Kigoma, na kusisitiza shirika hilo kwa kushirikiana na wakala wa usafiri wa majini na nchi kavu wako katika mchakato wa kuanzisha usafiri wa haraka wa abiria ambao utasimama katika vituo vikubwa pekee.



Picha: Ernest Nyambo

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments