[wanabidii] UZINDUZI WA REDIO JAMII UVINZA: MKUU WA MKOA AHIMIZA WELEDI, UADILIFU NA AMANI

Thursday, October 02, 2014
Habari za asubuhi,

Tafadhali pokea CODES, nikutakie siku njema.


<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><span style="color: #000080;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0177.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-118279" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0177.jpg" alt="DSC_0177" width="640" height="427" /></a></span></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mkuu wa Wilaya  ya Uvinza Mwalimu Hadijah Nyembo (kulia) akitoa nasaha zake kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya (wa pili kulia) kuzungumza na wakazi wa wilaya ya Uvinza kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo cha redio jamii Uvinza FM mkoani Kigoma. Kutoka kushoto ni Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi, Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambao ndio wadhamini wakuu wa redio Uvinza FM, Bi. Rose Haji Mwalimu na Mkurugenzi Mtendaji wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya.(Picha na Zainul Mzige wa MOblog).</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Na Mwandishi wetu, Uvinza - Kigoma</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya amesisitiza uadilifu katika vyombo vya habari jamii kwa kutangaza habari zisizoumiza hisia kwa wananchi wengine na kuepuka migogoro.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Akizindua kituo cha redio jamii cha Uvinza FM, Luteni Kanali Mstaafu Machibya alisema kuwa vyombo vina wakati mgumu hasa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2015.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong> "Changamoto hii  inaweza kuepukika kwa kuhakikisha habari zinazotolewa zinalenga kuendeleza utamaduni wa amani, upendo, utulivu na uvumilivu na kuepuka viashiria vinavyoweza kusambaza chuki  kwa lengo la kufanikisha chaguzi salama.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Mkuu wa Mkoa huyo amesisitiza umuhimu wa kuutumia uhuru wa kutoa na kupata habari vizuri kwa kusema kwamba uhuru huo usitumike kutoa habari zinazopendelea upande mmoja na kukandamiza mwingine kwa kuwa hali kama hiyo husababisha machafuko.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>"Kwa mujibu wa Ibara ya 18 (b) ya Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, kila mtu anayo haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari bila ya kujali mipaka ya nchi, lakini haki hiyo iende sambamba kwa kuzingatia Sheria za nchi na kuhakikisha habari hizo haziumizi hisia za wananchi wengine,"</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0206.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118274" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0206.jpg" alt="DSC_0206" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong> Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akisoma risala wakati wa uzinduzi wa kituo cha redio jamii Uvinza FM ambapo alilipongeza shirika la UNESCO kwa juhudi kuwaweka karibu wananchi na serikali kupitia mawasiliano ya redio.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya ameitaka redio jamii Uvinza kuonyesha uwezo wao ili waweze kujitangaza na kujijengea imani kwa wanajamii wao kuwa wanaweza. "Ni kwa hali hiyo tu mtaweza kujulikana, kutambulika na kupata udhamini na matangazo ya kutosha."</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Amewataka wanajamii kukitumia vyema kituo chao cha redio ili kiwe chachu ya kuleta na kukuza maendeleo katika vijiji, wilaya, mkoa na taifa kwa ujumla.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Wakati huo huo  Mkuu wa Mkoa ameitaka redio jamii ya Uvinza kutangaza habari zenye kuonyesha madhara ya mila potofu na kujenga uelewa wa jamii kuhusu mila hizo hususan mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), kufichua wagonjwa wanaohofia kuwa na dalili za ugonjwa wa ebola na uharibifu wa mazingira.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Amelipongeza shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kutoa msaada wa vifaa vya kituo hicho na kuendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo wanahabari jamii, Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kuruhusu matangazo ya Uvinza FM Redio yarushwe kupitia mnara wake na waanzilishi wa kituo hicho.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0120.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118275" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0120.jpg" alt="DSC_0120" width="640" height="444" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong> Mwalikishi wa Shirika la Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambaye pia ni mshauri na mkufunzi wa redio jamii, Bi. Rose Haji Mwalimu akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO Tanzania, Zulmira Rodrigues kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo hicho cha redio jamii Uvinza FM uliofanyika wilayani Uvinza mkoani Kigoma.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>"Ninayapongeza mashirika hayo ya Umoja wa Mataifa na Airtel kwa ufadhili wao, Ruchugi Salt Works na Asasi za kiraia (EHENA) kwa ushirikiano wao kwa jambo hili"</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong> Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya  ya Uvinza Mwalimu Hadijah Nyembo amewakumbusha waandishi wa habari kuepuka kutangaza habari zinazoleta hofu katika jamii kwa kutangaza habari zinazotoa maelezo ya ufafanuzi kutoka chombo husika.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Amekemea matumizi ya lugha isiyo sahihi na kutoeleweka kwa wasikilizaji kwa kusema kwamba redio inalenga makundi yote ya umri kwa hiyo Matangazo yalenge wananchi wote.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>"Redio Uvinza isiwe chombo cha propaganda, zingatieni mojawapo ya madhumuni ya kuanzishwa kwa redio zenu ambayo yanalenga kuhamasisha mshikamano, Amani, upendo, utulivu, umoja na utaifa, alisema Mwalimu Nyembo."</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Chombo cha habari jamii Uvinza FM Redio ni cha kwanza kuanzishwa mkoani Kigoma katika halmashauri mpya ya Uvinza.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0153.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118277" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0153.jpg" alt="DSC_0153" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><span style="color: #0000ff;">"Hongereni sana UNESCO serikali inatambua mchango wenu"</span>,...... Ni maneno ya  Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akimpongeza Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambao ndio wadhamini wakuu wa redio jamii Uvinza FM, Bi. Rose Haji Mwalimu  kwa niaba ya UNESCO. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Chombo hicho kimetakiwa kutumika  kuwaunganisha wanajamii, kuepuka kutangaza hisia au uvumi kwa kueleza ukweli na kuwatunzia heshima wasikilizaji wao kwa kuwa wana haki ya kuheshimiwa na kutoumbuliwa masuala yao binafsi.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Uzinduzi huo umeshuhudiwa pia na Mkuu wa wilaya ya Uvinza Mheshimiwa Mwalimu Hadijah Nyembo, viongozi wa chama na serikali, viongozi wa dini, Shirika la Umoja wa Mataifa (UNESCO), Kampuni ya simu za mkononi AIRTEL, wanakijiji na wananchi wa halmashauri ya Uvinza.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Wengine ni wanahabari 30 wanaohudhuria mafunzo ya maadili, jinsia na habari za migogoro kijijini Uvinza, kutoka redio jamii za wilaya 8 ambazo ni Karagwe, Bunda, Mwanza, Kahama, Sengerema, Maswa, Simanjiro, Loliondo, Mpanda, Ngara. Kutoka Zanzibar ni Unguja North, na Southern Pemba (Pemba).</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_00821.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118278" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_00821.jpg" alt="DSC_0082" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi, akitoa salamu kwa wakazi wa wilaya ya Uvinza kutoka kampuni ya simu za mkononi ya Airtel ambao wametoa udhamini wa mnara wao kurusha matangazo ya kituo cha redio jamii Uvinza FM ili kupanua wigo wa usikivu kwa redio hiyo.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0257.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118280" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0257.jpg" alt="DSC_0257" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong> Mkurugenzi Mtendaji wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya akitoa neno la shukrani kwa mkuu wa mkoa na wadhamini wa kituo hicho cha redio jamii Uvinza FM.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0054.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118293" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0054.jpg" alt="DSC_0054" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi akishiriki kutoa burudani na kikundi cha wakinamama wachimba chumvi Uvinza.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0164.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118281" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0164.jpg" alt="DSC_0164" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Baadhi ya viongozi wa dini na jeshi la polisi waliohudhiria uzinduzi huo...Kutoka kulia ni Sheikh Mkuu wa wilaya ya Uvinza Hassan Hamisi, OCD wa Wilaya ya Uvinza S.P Nobert Mahala, Mchungaji wa SDA, Pius Mutani, Mchungaji wa EAG Uvinza, Daniel Magunge na Diwani wa kata ya Ngumka, Abdallah Masanga.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0333.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118290" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0333.jpg" alt="DSC_0333" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Baadhi ya waandishi wa habari kutoka redio mbalimbali za jamii waliokuwa wakihudhuria warsha ya siku nane iliyokuwa ikiendelea kwenye kituo cha redio jamii Uvinza FM na wakazi wa wilaya hiyo waliohdhuria sherehe za uzinduzi wa kituo hicho.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0231.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118291" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0231.jpg" alt="DSC_0231" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0226.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118292" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0226.jpg" alt="DSC_0226" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0264.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118282" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0264.jpg" alt="DSC_0264" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kituo cha redio jamii Uvinza FM chini ya ufadhili wa Shirika la UNESCO na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania. Wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kulia ni Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi, Mwalikishi wa Shirika la Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambaye pia ni mshauri na mkufunzi wa redio jamii Bi Rose Haji Mwalimu pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0267.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118283" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0267.jpg" alt="DSC_0267" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong> Sasa kimezinduliwa rasmi.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0285.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118284" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0285.jpg" alt="DSC_0285" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akifanyiwa mahojiano mafupi ndani ya studio za redio jamii Uvinza FM na Mtangazaji wa kituo hicho, Kadisilaus Simon mara baada ya kuzindua rasmi redio hiyo.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0304.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118285" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0304.jpg" alt="DSC_0304" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akisaini kitabi cha wageni ndani ya studio za redio jamii Uvinza FM.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0308.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-118286" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/10/DSC_0308.jpg" alt="DSC_0308" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mtangazaji wa kituo cha redio jamii Uvinza FM, Kadisilaus Simon akitekeleza majukumu yake kwa furaha kabisa mara baada ya kupewa baraka na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya.</strong></em></span></p>

KAWAIDA

DSC_0177

Mkuu wa Wilaya  ya Uvinza Mwalimu Hadijah Nyembo (kulia) akitoa nasaha zake kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya (wa pili kulia) kuzungumza na wakazi wa wilaya ya Uvinza kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo cha redio jamii Uvinza FM mkoani Kigoma. Kutoka kushoto ni Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi, Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambao ndio wadhamini wakuu wa redio Uvinza FM, Bi. Rose Haji Mwalimu na Mkurugenzi Mtendaji wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya.

Na Mwandishi wetu, Uvinza - Kigoma

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya amesisitiza uadilifu katika vyombo vya habari jamii kwa kutangaza habari zisizoumiza hisia kwa wananchi wengine na kuepuka migogoro.

Akizindua kituo cha redio jamii cha Uvinza FM, Luteni Kanali Mstaafu Machibya alisema kuwa vyombo vina wakati mgumu hasa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2015.

 "Changamoto hii  inaweza kuepukika kwa kuhakikisha habari zinazotolewa zinalenga kuendeleza utamaduni wa amani, upendo, utulivu na uvumilivu na kuepuka viashiria vinavyoweza kusambaza chuki  kwa lengo la kufanikisha chaguzi salama.

Mkuu wa Mkoa huyo amesisitiza umuhimu wa kuutumia uhuru wa kutoa na kupata habari vizuri kwa kusema kwamba uhuru huo usitumike kutoa habari zinazopendelea upande mmoja na kukandamiza mwingine kwa kuwa hali kama hiyo husababisha machafuko.

"Kwa mujibu wa Ibara ya 18 (b) ya Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, kila mtu anayo haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari bila ya kujali mipaka ya nchi, lakini haki hiyo iende sambamba kwa kuzingatia Sheria za nchi na kuhakikisha habari hizo haziumizi hisia za wananchi wengine,"

DSC_0206

 Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akisoma risala wakati wa uzinduzi wa kituo cha redio jamii Uvinza FM ambapo alilipongeza shirika la UNESCO kwa juhudi kuwaweka karibu wananchi na serikali kupitia mawasiliano ya redio.

Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya ameitaka redio jamii Uvinza kuonyesha uwezo wao ili waweze kujitangaza na kujijengea imani kwa wanajamii wao kuwa wanaweza. "Ni kwa hali hiyo tu mtaweza kujulikana, kutambulika na kupata udhamini na matangazo ya kutosha."

Amewataka wanajamii kukitumia vyema kituo chao cha redio ili kiwe chachu ya kuleta na kukuza maendeleo katika vijiji, wilaya, mkoa na taifa kwa ujumla.

Wakati huo huo  Mkuu wa Mkoa ameitaka redio jamii ya Uvinza kutangaza habari zenye kuonyesha madhara ya mila potofu na kujenga uelewa wa jamii kuhusu mila hizo hususan mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), kufichua wagonjwa wanaohofia kuwa na dalili za ugonjwa wa ebola na uharibifu wa mazingira.

Amelipongeza shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kutoa msaada wa vifaa vya kituo hicho na kuendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo wanahabari jamii, Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kuruhusu matangazo ya Uvinza FM Redio yarushwe kupitia mnara wake na waanzilishi wa kituo hicho.

DSC_0120

 Mwalikishi wa Shirika la Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambaye pia ni mshauri na mkufunzi wa redio jamii, Bi. Rose Haji Mwalimu akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO Tanzania, Zulmira Rodrigues kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo hicho cha redio jamii Uvinza FM uliofanyika wilayani Uvinza mkoani Kigoma.

"Ninayapongeza mashirika hayo ya Umoja wa Mataifa na Airtel kwa ufadhili wao, Ruchugi Salt Works na Asasi za kiraia (EHENA) kwa ushirikiano wao kwa jambo hili"

 Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya  ya Uvinza Mwalimu Hadijah Nyembo amewakumbusha waandishi wa habari kuepuka kutangaza habari zinazoleta hofu katika jamii kwa kutangaza habari zinazotoa maelezo ya ufafanuzi kutoka chombo husika.

Amekemea matumizi ya lugha isiyo sahihi na kutoeleweka kwa wasikilizaji kwa kusema kwamba redio inalenga makundi yote ya umri kwa hiyo Matangazo yalenge wananchi wote.

"Redio Uvinza isiwe chombo cha propaganda, zingatieni mojawapo ya madhumuni ya kuanzishwa kwa redio zenu ambayo yanalenga kuhamasisha mshikamano, Amani, upendo, utulivu, umoja na utaifa, alisema Mwalimu Nyembo."

Chombo cha habari jamii Uvinza FM Redio ni cha kwanza kuanzishwa mkoani Kigoma katika halmashauri mpya ya Uvinza.

DSC_0153

"Hongereni sana UNESCO serikali inatambua mchango wenu",...... Ni maneno ya  Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akimpongeza Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambao ndio wadhamini wakuu wa redio jamii Uvinza FM, Bi. Rose Haji Mwalimu  kwa niaba ya UNESCO. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya.

Chombo hicho kimetakiwa kutumika  kuwaunganisha wanajamii, kuepuka kutangaza hisia au uvumi kwa kueleza ukweli na kuwatunzia heshima wasikilizaji wao kwa kuwa wana haki ya kuheshimiwa na kutoumbuliwa masuala yao binafsi.

Uzinduzi huo umeshuhudiwa pia na Mkuu wa wilaya ya Uvinza Mheshimiwa Mwalimu Hadijah Nyembo, viongozi wa chama na serikali, viongozi wa dini, Shirika la Umoja wa Mataifa (UNESCO), Kampuni ya simu za mkononi AIRTEL, wanakijiji na wananchi wa halmashauri ya Uvinza.

Wengine ni wanahabari 30 wanaohudhuria mafunzo ya maadili, jinsia na habari za migogoro kijijini Uvinza, kutoka redio jamii za wilaya 8 ambazo ni Karagwe, Bunda, Mwanza, Kahama, Sengerema, Maswa, Simanjiro, Loliondo, Mpanda, Ngara. Kutoka Zanzibar ni Unguja North, na Southern Pemba (Pemba).

DSC_0082

Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi, akitoa salamu kwa wakazi wa wilaya ya Uvinza kutoka kampuni ya simu za mkononi ya Airtel ambao wametoa udhamini wa mnara wao kurusha matangazo ya kituo cha redio jamii Uvinza FM ili kupanua wigo wa usikivu kwa redio hiyo.

DSC_0257

 Mkurugenzi Mtendaji wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya akitoa neno la shukrani kwa mkuu wa mkoa na wadhamini wa kituo hicho cha redio jamii Uvinza FM.

DSC_0054

Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi akishiriki kutoa burudani na kikundi cha wakinamama wachimba chumvi Uvinza.

DSC_0164

Baadhi ya viongozi wa dini na jeshi la polisi waliohudhiria uzinduzi huo...Kutoka kulia ni Sheikh Mkuu wa wilaya ya Uvinza Hassan Hamisi, OCD wa Wilaya ya Uvinza S.P Nobert Mahala, Mchungaji wa SDA, Pius Mutani, Mchungaji wa EAG Uvinza, Daniel Magunge na Diwani wa kata ya Ngumka, Abdallah Masanga.

DSC_0333

Baadhi ya waandishi wa habari kutoka redio mbalimbali za jamii waliokuwa wakihudhuria warsha ya siku nane iliyokuwa ikiendelea kwenye kituo cha redio jamii Uvinza FM na wakazi wa wilaya hiyo waliohdhuria sherehe za uzinduzi wa kituo hicho.

DSC_0231

DSC_0226

DSC_0264

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kituo cha redio jamii Uvinza FM chini ya ufadhili wa Shirika la UNESCO na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania. Wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kulia ni Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi, Mwalikishi wa Shirika la Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambaye pia ni mshauri na mkufunzi wa redio jamii Bi Rose Haji Mwalimu pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya.

DSC_0267

 Sasa kimezinduliwa rasmi.

DSC_0285

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akifanyiwa mahojiano mafupi ndani ya studio za redio jamii Uvinza FM na Mtangazaji wa kituo hicho, Kadisilaus Simon mara baada ya kuzindua rasmi redio hiyo.

DSC_0304

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akisaini kitabi cha wageni ndani ya studio za redio jamii Uvinza FM.

DSC_0308

Mtangazaji wa kituo cha redio jamii Uvinza FM, Kadisilaus Simon akitekeleza majukumu yake kwa furaha kabisa mara baada ya kupewa baraka na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya.


--
Zainul A. Mzige,
Operation Manager,
MO BLOG,
+255714940992.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Share this :

Related Posts

0 Comments